Tunaomba ushirikiano wako
Kwa yeyote mwenye taarifa, au mwenye uwezo wa kutusaidia, asubuhi ya leo, Jumapili, Oktoba 3, 2010, kwenye eneo la maegesho ya magari nje ya Kigango cha Mt. Thomas Moore, Ally Sykes Close, Mbezi Beach, takriban saa 4 za asubuhi, wakati misa ikiendelea, gari aina ya Suzuki Swift iliyokuwa kwenye eneo hilo ilivunjwa kioo cha nyuma na mlango wa nyuma kufunguliwa, hatimaye kuwezesha baadhi ya vitu vilivyokuwamo ndani yake kuchukuliwa na mtu au watu
wasiojulikana.
Tunajua utadhani kwamba huu ni mtego. La hasha. Tunachotaka ni vitu hivyo kurejeshwa kwani ni hasara kubwa sana kwetu. Tupo tayari kukuzawadia kwa ushirikiano wako, kwani hatuna muda wa kwenda kufungua kesi Polisi au Mahakamani, kwani tuna uhakika kwamba kwa njia hii HATUTAFANIKIWA. Tunachokuomba ni uaminifu wako na imani yako, kwamba, hatutachukua hatua zozote za kisheria.
Tafadhali turejeshee vitu vyote vilivyokuwamo ndani ya gari, tuko tayari kukupa kiasi kizuri cha pesa kama shukrani yetu kwako. Muda wa kuomba upya kadi ya benki ya CRDB, kutafuta kitambulisho kipya cha kazi, kutafuta kadi ya mpiga-kura huku zikiwa imebaki siku chache sana kabla ya Uchaguzi Mkuu, na hii ni muhimu zaidi, kumbukumbu za namba za simu na picha zilizopo kwenye simu za mkononi (ambazo thamani yake haihesabiki), vyote hatuna muda wa
kufuatilia, ni hasara kwetu.
Tunajua kwamba ni dhiki ndiyo inayokusumbua, na kwamba, unaona kwamba hiyo ndiyo njia sahihi kwako kujipatia chochote. Hatuwezi kukuhukumu kwa kuwa maskini!
Tafadhali wasiliana nasi kwa namba za simu
0715-019119 au 0786-019019
ili tuweze kukutana nawe na kurejeshewa vitu hivyo.
Asante.
Familia ya Bw. na Bibi Aziz Losika Mongi
P.S. Ni bora tukayamaliza kati yetu kuliko kupelekana Polisi, ambapo hatutapata muafaka!
Kwa yeyote mwenye taarifa, au mwenye uwezo wa kutusaidia, asubuhi ya leo, Jumapili, Oktoba 3, 2010, kwenye eneo la maegesho ya magari nje ya Kigango cha Mt. Thomas Moore, Ally Sykes Close, Mbezi Beach, takriban saa 4 za asubuhi, wakati misa ikiendelea, gari aina ya Suzuki Swift iliyokuwa kwenye eneo hilo ilivunjwa kioo cha nyuma na mlango wa nyuma kufunguliwa, hatimaye kuwezesha baadhi ya vitu vilivyokuwamo ndani yake kuchukuliwa na mtu au watu
wasiojulikana.
Tunajua utadhani kwamba huu ni mtego. La hasha. Tunachotaka ni vitu hivyo kurejeshwa kwani ni hasara kubwa sana kwetu. Tupo tayari kukuzawadia kwa ushirikiano wako, kwani hatuna muda wa kwenda kufungua kesi Polisi au Mahakamani, kwani tuna uhakika kwamba kwa njia hii HATUTAFANIKIWA. Tunachokuomba ni uaminifu wako na imani yako, kwamba, hatutachukua hatua zozote za kisheria.
Tafadhali turejeshee vitu vyote vilivyokuwamo ndani ya gari, tuko tayari kukupa kiasi kizuri cha pesa kama shukrani yetu kwako. Muda wa kuomba upya kadi ya benki ya CRDB, kutafuta kitambulisho kipya cha kazi, kutafuta kadi ya mpiga-kura huku zikiwa imebaki siku chache sana kabla ya Uchaguzi Mkuu, na hii ni muhimu zaidi, kumbukumbu za namba za simu na picha zilizopo kwenye simu za mkononi (ambazo thamani yake haihesabiki), vyote hatuna muda wa
kufuatilia, ni hasara kwetu.
Tunajua kwamba ni dhiki ndiyo inayokusumbua, na kwamba, unaona kwamba hiyo ndiyo njia sahihi kwako kujipatia chochote. Hatuwezi kukuhukumu kwa kuwa maskini!
Tafadhali wasiliana nasi kwa namba za simu
0715-019119 au 0786-019019
ili tuweze kukutana nawe na kurejeshewa vitu hivyo.
Asante.
Familia ya Bw. na Bibi Aziz Losika Mongi
P.S. Ni bora tukayamaliza kati yetu kuliko kupelekana Polisi, ambapo hatutapata muafaka!
Serikali na Wanakijiji wa Mitaa hasa hasa wanatakiwa waweke sungusungu kama Serikali hawafanyi kitu.
ReplyDeleteMie nashangaa Hasa maeneo ya huko Mbezi Kuna Kambi kibao za Wanajeshi na Kazi hawana kwanini hawapewi kazi za kulinda? au wao ndio Wezi? na wengi wakazi wa huko wanaibia mchana au usiku mida ya watu wanajirusha wengi watu wa kazi mjini wanasomwa.
MZ.
KWA KWELI HALI HII INATISHA,MAMBO YA AINA HII YATAISHA LINI NCHINI KWETU?HASA HAPO DAR?WATU HAWANA HATA UHURU WA KWENDA SEHEMU WAKATOKA SALAMA,LAZIMA HASARA HATA VIFO VITOKEE,IMEKUWA KAMA NDIYO STAILI YA MAISHA YA MTANZANIA.HATUJUI HATA WA KUMLAUMU.
ReplyDeletePOLENI SANA NDUGU MLIOIBIWA MALI ZENU,INASIKITISHA SANA KWANI PAMOJA NA UMASKINI ULIOKITHIRI KATIKA NCHI YETU,HUU SIYO USTAARABU HATA KIDOGO.
MDAU, LONDON
HIIKALI YAKE,KULINGANA NA MAELEZO YA MLETA MADA YAELELKEA WANAWAJUA WEZI WAO SASA HAWATAKI KUWAPELEKA POLISI KWA KUWA NI KUPOTEZEANA MUDA,SASA KAMA UNAWAJUA SI UWAPELEKE KWA PILATO TU,SASA HAPA HUPUNGUZI WEZI UNAONGEZA VIBAKA,
ReplyDeletedah!poleni sana.ila sidhani kama wezi /vibaka wa tanzania wameelimika kiasi cha kutumia teknologia ya matandao wa intanet.muhimu tangazeni redion au kwenye runinga, huo ni ushauri wa bure.
ReplyDeleteHii ni approach nzuri iliyotumika ila neno dhiki nikama kashfa!
ReplyDeleteNahawa vibaka hawana access na mtandao.Ni vizuri ukawatangazia vijana wanaofanya shughuli zao jirani na tukio lilipotokea au vijiwe vya wahuni viliopo jirani.
Pole sana.Usikate tamaa utavipata tu.
UNBELIEVABLE!!! Be carefull what you say,it mighty come back and HAUNT YOU!!
ReplyDeleteMIMI inaonekana nimekaa nje sana,hivyo vibaka wa bongo siku hizi wanasoma internet,maana sielewi huu ujumbe utamfikia vipi
ReplyDeleteKWELI BONGO AMANI HAKUNA KABISA.SASA ONA WATU HAWANA AMANI NA MALI ZAO,PIA HATA WATAFUTA HAKI NAO HAWANA IMANI NA VYOMBO VYA DOLA.......KWAKWELI HALI INASIKITISHA KILA NIKIONA MATUKIO YA AINA HII, HALAFU TUNAJIVUNIA AMANI, AMANI GANI HUKU WATU HAWANA AMANI NA MALI ZAO?????
ReplyDeletePoleni sana Bw na Bi Mongi kwa upotevu wa mali zenu.Mimi nakaa Mbezi na eneo hilo nalifahamu.
ReplyDeleteHata hivyo ushauri wangu ni huu:
-sidhani kama mhalifu aliyetenda hili anauwezo wa kupitia blog kama hizi
-nimepita hapo na naona mnajenga fence, je mna walinzi hapo?
=kama walinzi wapo, uzoefu unaniambia wanahusika sana
-kanisani kwetu KKKT Mbezi huwa walinzi wanakuwa liable kwa loss yoyote ya mali ya msharika wakati wa ibada,losses zikawa minimized baada ya walinzi kutozwa upotevu.
Siwaungi mkono hao vibaka, lakini kwani uache au utembee na vitu vyote kwenye gari wakati unajua kabisa vikiibiwa ni viguu kuvi-replace? Hata kadi ya benki unaacha kwenye gari? Kwa kweli hapo unategemea nini? Kama gari ilikuwa tupu sidhani kama wangevunja. Hata huku Ulaya ukiacha hivyo vitu kwenye gari unavunjiwa. Sembuse bongo.
ReplyDeleteduh,poleni sana,serikali ipo busy na kampeni,mda wa kuwalinda raia haupo.jaribu kuongea na watoto wa vijiweni unaweza kuvipata,Tanzania amani hakuna kabisa,mungu aturehemu tu.
ReplyDeleteduh,poleni sana,serikali ipo busy na kampeni,mda wa kuwalinda raia haupo.jaribu kuongea na watoto wa vijiweni unaweza kuvipata,Tanzania amani hakuna kabisa,mungu aturehemu tu.
ReplyDeleteHUWEZI KUHUKUMU KWA KUWA MASKINI!!!?? WEE UNAONEKANA UNA DHARAU SANA. JUST BECAUSE MUNGU AMEKUJALIA KWA KUWA NA KIJIUWEZO!? KWANZA TAMBUA ONLY GOD CAN JUDGE! wee huna uwezo wa kumhukumu mtu, na kumwita mtu MASKINI!!! jifunze vizuri tafsiri ya maskini kabla ya kutumia.
ReplyDeletepamoja na kuwa umechukuliwa vitu, polite approach ingesaidia. kuliko kashfa hizo ulizotumia. hata ningekuwa mimi nimeiba nisingerudisha. maana unajidai sana wewe. Wabongo bwana! kiji uwezo kidogo tu basi madharau kibao!
Kama alivosema mdau hapo juu tangaza dau nono vijiwe vya hapo karibu utapata vitu vyako mi niliibiwa hivyo laptop mbili,documents na vingine kadhaa na nikavipata kwa kotoa elfu hamsini tu sidhani tumefika wadokozi kusoma michuziblog.
ReplyDeleteHalafu CCM wanazunguza kuuliza wananchi "Tuna amani hatuna?" na wananchi wanajibu "tunayo!!!!" Haya ni masikitiko makubwa ndugu zangu, ukweli ni kwamba hatuwezi tukawa kwenye amani kama idadi kubwa na wanachi wamegubikwa na umaskini mkubwa!!!!! Michuzi najua unabana sana maoni kama haya yanayofichua chanzo cha matatizo....ukweli wa mambo hapa ni kwamba CCM tuwamwage tu, ili tusonge mbele na kujenga nchi yetu na hatimaye kupata amani ya kweli. Michuzi bana tu, lakini ujumbe unakufikia na lazima ujue kuwa unaangamiza nchi yako, kwa kuendelea kufagilia CCM na serikali yake kwa maslahi yako binafsi!! Mimi sina shida hata kidogo, na ningekuwa ni mbinafsi kama wewe, basi ningekuwa sina sababu yeyote ya kuipinga CCM, kwani kuwepo kwao madarakani au kutokuwepo mimi napeta tu. Tatizo ni ndugu zangu waTanzania waliowengi ambao wamegubikwa na umaskini mkubwa na CCM imeshidwa dhahiri kuondoa umaskini huo.
ReplyDeleteNi mimi Muungwana
USA
BONGO BALAA MWEZI ULIOPITA NILIKUWA HUKO MZEE NIMEFUNGA VIOO VIBAKA WALICHUKUA SIGHT MIRRORS ZOTE KAMA KUPANGUSA SIKUAMINI UTADHANI WAMESOMEA.
ReplyDeletePole sana unaweza kufanikiwa kwa njia hii, ila kejeli kwamba dhiki zisumbua zinaweza kutafsiriwa vengine na hawa vibaka, kuna vibaka ni High tech na wala hawana dhiki ivo, rekebisha usemi ili mlengwa/walengwa wakuonee huruma, kwa kusema ni dhiki kibaka atakuona ni arrogant na una madharau.
ReplyDeleteJamani kabla hujatuma maoni tufikiri kwanza, wewe Anony Sun Oct 03,06:17:00pm. Internet haisomwi ila habari zinasomwa kwenye Internet. Jamani hata kiswahili kinatushinda? Ni hayo tu.
ReplyDeleteACHA ZARAU WEWE UNANIITA NAZIKI THEN UNATAKA NIKURUDISHIE , LOL UNACHEKESHA .
ReplyDeleteHALAFU BADO MNA WACHAGUA VIONGOZI BOMU , UKIONA VITENDO KAMA HIVI HINA MAANA HALI NGUMU SANA! ALAFU WEWE MTOA TANGAZO HINAONEKANA JAMAA WAMEAMUA TU KUKU KOMESHA KWANI UNAONEKANA WEWE NI MTU WA ZARAU SANA UTAWAHITAJI BINADAMU WENZAKO WANA ZIKI WEWE UNA NINI SASA ? KAMA WEWE UMEVIMBIWA BASI TULIA WENYE ZIKI WALE
ReplyDeleteMDAU FROM PARIS
AKUNA VIBAKA WENYE ZIKI UKU !!
lazima kujifunza kutokuweka vitu garini vitapoonekana, ni kuacha gari kama vile hakuna kitu hata ukificha chini ya kiti angalia isionekane na hii tunafanya miaka mingi sio hapo tu dar hata ulaya ni hivyo watu wanafanya.
ReplyDeletepia ukijua unaenda sehemu anza ficha kabla ujafika kupaki gati as wezi watakuwa lazima wanavizia kuona ukichelewa au kujionyesha unaweka vitu vizuri unalo.
ila kama kuna wanaokaa maeneo hayo wauzaji walinzi kama wapo lazima anayejua kilichoendelea.
ni kweli inaonekana unawajua nani kaiba, basi wafate waambie wakurudishie, au hii ni matatizo ya kifamilia au boy/girlfriend kufanyiziana, maana ni kama unaona umechaguliwa wewe kwa makusudi.
WENGI WANAWAJUWA WANAFANYIANA U MAFIA BONGO SIKU HIZI MTU ANAMPOTEZA MWENZAKE VIBAYA KIMAFIA NI DEAL ZAO ZIKIENDA VIBAYA AU WAKICHUKULIANA MADEMU BASI STORI TU HAPO JUU UTAONA NA WENGI WANAOKAA MITAA HIYO.
ReplyDeleteJE KUNA MDAU ANANIUNGA MKONO? MAKIZINGA.
Pole sana , but I think vibaka hawasomi humu.tumia akili nyingine.
ReplyDeleteHatuwezi kukuhukumu kwa kuwa maskini! - DUH HILO TUSI SASA....
ReplyDeleteIdle threat aka mkwara mbuzi hata ningekua mimi ndo mwizi nisingerudisha, my advise to you just go tanga mkatafute sangoma labda mtafanikiwa but your approach on this is unattainable!!
ReplyDeletePole sana ndugu kwa kuibiwa! huo uamuzi wako wa kutokwenda polisi mimi nauunga mkono, kwani utapoteza muda wako bure!! polisi wetu ni bomu! tena wanakula nao hao vibaka!! nakuombea tu upate vitu vyako muhimu!
ReplyDeleteIs this for real or is just an indirect message? Hao vibaka kweli wanasoma blog ya jamii siku hizi au ni vibaka wengine (Mafisaid) ...
ReplyDeleteKuita mtu ana dhiki sio vyema kabisa kwa vile hujui yaliyomsibu hyo mwizi. Niishi na vibaka wengi tu ambao ni watoto wa matajiri sana Tanzania. Hivi mafisadi wakichukua hela unadhania ni dhiki?
usiie watuw anadhiki kwa vile kuiba sio dhiki..
kutokana na sifa njema ulizomwagia, za udhiki na umasikini wake,
ReplyDeleteakirudisha "FALA".
hahahaha!!! Jamaa ana mikwara duuh!!! hayo maneno tu baba hata kwenye Khanga yapo,Cha kukushauri hapa zama maskani ya karibu na tukio tangaza dau wana watakurudishia.Na upunguze ukali kwenye ishu kama hizi Simba mwenyewe na ukali wake wote bado watu wanamnywesha chai
ReplyDeleteoya mwana ngoja nikuhabarishe,unajua nini bro?sie juzi hatukuwa na mapene si ndo tukaona tulianzishe?kupita kitaa tu tukaona mkoko wako,sema nini bro una mazarau kwa sana tu,wewe na demu wako hapa kitaa mmekuwa watu wa ngendengwe kwa sana tukaona tutafte shavubhumo garini so tukalianzisha!sasa humu ndani tumelamba laputopu yako,vilongalonga vya kiukweli na hizi kadi zako pia kuna mapene sasa sie kama vp mwana tunakuletea kiuzushi hapo mjengoni haya mazagazaga kama kadi za benki,za kura na wanja wa bidada na mkoba wake sie tunajisevia kiuzushi mpango mzima ila usijaribu kuwaabia hawa mastono wa kova noma mwana japo samtaime tunashirikiana nao huku kitaa kwa sana ila umetuzalilisha hapa mtandaoni,lakini aliamudulilai hii lapatopu yako inatutoa kwani leo tumeweza kusafu mtandaoni,nasi tunatesa kama vp nikong`otee kilongalonga changu namba 0718 12 341
ReplyDeleteAHSANTE BY KIBAKA MSOMI
MBEZI BEACH.
ahahahaha mm nimefurahi ulivyoibiwa wajua kwanini?dharau imekuwa kubwa sana eti maskini unaijua tafsiri ya masikini wewe?yaani bora walivyokuibia dharau ikuishe
ReplyDeletenajua ume-post hapa ukijua kabisa si sehemu husika kutangaza hizi habari na pia approach uliyotumia hakuna kibaka yoyote duniani anayeweza kuthubutu kupiga simu wakati siku hizi simu zimesajiriwa
ReplyDeletekingine umeonesha dharau kwa kumwita kibaka kuwa ni masikini na pia ana dhiki, kumbuka kuwa hata gari yako uliyotaja ni ya kimasikini pia elewa kuwa nchi yetu ni masikini hivyo wananchi wake nao ni masikini pia kwa hiyo na ww ni masikini wa mali na roho maana kanisani ulitakiwa kwenda na vogue sio Suzuki Swift gari ya bei rahisi
Ushauri:
weka alarm kwenye gari yako, pia usipende kutembea na vitu kwenye gari ambavyo una matumizi navyo kwa wakati huo kama kitambulisho cha kupigia kura, cha ofisini n.k au kama vinabebeka tembea navyo sio unaweka kwenye gari matokeo yake ndio hayo, tafuta njia nyingine za kidiplomasia za kutafuta hivyo vitu na pia unapopiga picha kwenye simu uwe unazitoa na kuhifadhi kwenye CD au kuzisafisha kama ni muhimu sana, kuhusu uchaguzi pole kura yako haitakuwepo (hapo ndio issue kwa taifa)
Ushauri mwingine: Muache dharau kwa watu hata kibaka nae ni mtu tena huyo ni bora zaidi ya fisadi
Aliyekuambia kuwa vibaka wa siku hizi ni maskini amekuongopea... Nenda Slipway, CocoBeach, Makabirini wakati wa Kuzika, Mlimani City, na hata Diamond Jubilee uone vibaka wanaokuja na Magari mazuri na wanapaki jirani na gari yako ndipo wanavunja vioo na kuiba. Tena kuna watoto wa Kiarabu na wahindi ambao kutokana na imani zetu kuwa ni matajiri na sio wezi, basi wakiegemea gari yako wapita njia wanajua yao, hivyo wanakuibia kirahisi sana...
ReplyDeletePole kwa yaliyo kukuta, kawahi kufunga acount zako maana siku hizi watu wanahitaji kujua akaunti namba yako tu bila password...
Allo wewe KIBAKA MSOMI wa Mbezi Beach,
ReplyDeleteMbona namba yako ya simu haijatimia herufi zote? Au walikufundisha tu kusoma lakini sio kuhesabu?
Kama kweli unayo nia ya kusaidia, basi uitimize hiyo nia ipasavyo, au sio?
aisee yani awa jamaa wana adi funguo malaya automatic wakibonya tu magari zaidi ya 1 yanaungua na wanabeba vitu kiulaini
ReplyDeletetanzania tuiombee tunakoelekea siko,na ivi shilingi inazidi kuzama
Mtoa mada ameleta kilio chake kwa wanalibeneke akiamini yamefika mmojawetu hivyo ajaribu kutoa maelekezo alichukua hatua gani hadi kupata vitu alivyoibiwa. tatizo ni kwamba, badala ya kutoa ushauri baadhi ya watu wanatoa maoni yanayoprovoke badala ya kumconfort mtoa mada. Ni bora kukaa kimya kuliko kufanya ambayo wengi wetu hufanya, kuandika hata kama ni utumbo. Au wengi wa waandikaji ni vijana wa skuli waliochoropoka kutoka maskulini buguruni kwa madenge, mburahati mianzini au tandale kwa mfuga mbwa? shiiiiiiiiiiit!
ReplyDelete"Tunajua kwamba ni dhiki ndiyo inayokusumbua, na kwamba, unaona kwamba hiyo ndiyo njia sahihi kwako kujipatia chochote. Hatuwezi kukuhukumu kwa kuwa maskini!" nimechoka na hilo nimeona ni nunukuu kama ilivyo...hizi jeuri??????
ReplyDeleteKwa mtindo huu uliokuja nao utaendelea kuibiwa kila siku, kwanza kashfa kuwaita wenzio maskini,na kutumia lugha ya kutisha..sema umeishiwa cha kusema ndo maana usema hutaki kwenda polisi. Jifunze kutumia lugha ya kistaarabu ili usaidiwe..acha ulimbukeni!
ReplyDelete