Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiendesha trekta aina ya FARMTRUCK kutoka India wakati alipozindua Mradi wa Matrekta ya Kilimo Kwanza unaosimamiwa na SUMA JKT. Uzinduzi huo umefanyika leo kwenye eneo la kambi ya Jeshi ya Lugalo Mjini Dar es salaam.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika mazungumzo na Balozi wa India Nchini,V. Bhagirathi wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Matrekya ya Kilimo Kwanza unaosimamiwa na SUMA JKT. Uzinduzi huo umefanyika leo kwenye eneo la kambi ya jeshi ya Lugalo ya jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Matumizi ya matrekta katiaa kilimo ili kuongeza tija ni jambo lisilokwepeka. Lakini pamoja na hiyo tija tuangalie athali yake kw mazingira namabadiliko ya hali ya hewa. wengi tunakumbuka jinsi Isimani ilivyokuwa ikzalisha chakula kwa wimgi wakitumia matrekta. Wakakata miti bila mpangilio, leo hii jangwa linainyemelea. Hivyo upanuzi na usafishaji wa mashamba ili matrekta yaweze kufanya kazi uende sambamba nakuhakikisha miti inahifadhiwa au kupandwa kama ilivyo kwenye mashamba ya kahawa. Hili litatuhakikishia uendlevu wa uzalishaji na tija. Tuige huko watumiako matrekta kwa wingi

    ReplyDelete
  2. Ni jambo jema kuwa na matrekita kwa ajiri ya kilimo lakini wasi wasi yangu matreketa kutokea India. Nisemapo India siyo kwamba nawabeza kwa technologia bali hawa watu wanajua kuchakachua sana. Na wanarecord ya kutuuzia vitu vizee na kuvipaka rangi. kama kumbu kumbu inanipeleka vizuri hata ndege ya ATC iliyoletwa kwa kupitia kwa wahindi ilikuja kuwekwa kwenye mawe miaka hiyo ya 1980s, madawa mengi ya binadamu yanayotoka India tunajua wote

    ReplyDelete
  3. Soma pia au angalia documentary ya madhara ya kilimo India. Kumbuka siyo matrecter tu watalet na vinginevyo labda vipo njiani. Madhara ya kilimo chao ni makubwa sana, kama ukiangalia miaka 10 au 20 ijayo. Tatizo letu sisi wasomi wapo wengi wa kilimo lakini hakuna hata mmoja kijijini. Na kwa ajili hiyo ni nani atakayesimamia hicho kilimo. Ukishapata kadigree kila mtu antaka kwenda nje aje aishi mjini na badala ya kwenda kijiji kuishi na wakulima au wafugaji. Kama mnabisha niambieni ni mtaalamu gani yupo kijijini siku ya leo. Kazi kwetu tutatupiwa kila kitu na hakuna kualalamika kwani tumeijenga hiyo hali siis wenyewe.

    ReplyDelete
  4. Huu ndio Mradi wa Shambo?

    ReplyDelete
  5. areeee bayaaaa... veve na sema nini ? india iko baya ? veve naweza tengeza trekta ? veve uweziii kabisaaa bayaaa... veve naweza kupiga kelelele tuuuuu bayaaa


    mdau muhindi from india

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...