Marehemu Edwin Magesa Mwema

Familia ya Mwema wa Tarime Musoma wanapenda kutoa shukrani kwa Ndugu Jamaa na Marafiki walioshirikiana nasi katika kipindi hiki kigumu cha kuomboleza msiba wa Kijana wetu mpendwa Edwini Magesa Mwema Kilichotokea jumapili Tarehe 24/10/2010 na hatimaye kuzikwa leo Tarehe 28/10/2010 kijijini Tagota - Tarime.

Sio rahisi kumshukuru mmoja mmoja lakini Familia inatoa Shukrani za kipekee kwa Uongozi na Wafanyakazi wa CRDB (Ambako marehemu alikuwa akifanya kazi) kwa ushirikiano mkubwa waliotupatia tangu Kifo mpaka Mazishi, Madaktari na wauguzi wa Agha Khan Hospital.

Ndugu, Jamaa na Marafiki wote...
Familia haina cha kuwalipa ila kuwaombea kwa Mungu.
Tunashukuru kwa Faraja zetu na Sala Zenu.
Bwana alitoa, Bwana Ametwaa -
Jina la Bwana Lihimidiwe
AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 28 mpaka sasa

  1. Poleni sana wafiwa katika kipindi hiki kigumu. Neno la bwana linasema shukuruni kwa kila jambo. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe

    ReplyDelete
  2. R.I.P Magessa,

    ReplyDelete
  3. POLENI SANA

    NIMESHTUKA SANA, KIJANA NILIKUWA NA JUA KWANI NILIMUACHA MLIMA PALE WAKATI ANASOMEA BCOM. PIA BAADA YA HAPO TULIKUWA TUNAKUTANA MITAANI KULE KIMARA NA MJINI HASWA PALE AZIKIWE.

    ReplyDelete
  4. Du poleni sana ngugu familia hivi sijuwi hawa kina magesa ni ndio wale wa dodoma eria C sijuwi ? naombeni ufafanuzi ndugu familia . poleni sana familia tupo pamoja nanyi

    ReplyDelete
  5. RIP Mwema.

    ReplyDelete
  6. Gone too soon Mwema, I was shocked!. You lived your life well, you were a great friend, you started climbing corporate ladder at a very young age. I will miss you my buddy. RIP Mwema!

    ReplyDelete
  7. Tulikuwa naye na kushirikiane naye kwa mambo mengi, hakika alikuwa mtu mwema kama lilivo jina lake. Nilimjua zaidi tulipokuwa pamoja chuo cha Diplomasia kurasini 2005/6.

    KWa hakika tumepoteza kijana muhimu, ila kazi ya Mungu haina makosa. yeye ametangulia na sisi tutafuatia.

    Diplomat.

    ReplyDelete
  8. RIP Mwema....oh God; Rest in Peace Mwema!

    ReplyDelete
  9. Very shocking news indeed!!. RIP my classmate Mwema, he was really Mwema. Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina lake lihimidiwe.

    ReplyDelete
  10. RIP kaka duh nimeshituka sana kuona hii habari...

    ReplyDelete
  11. Ah! I am shocked!

    He was a good friend of mine at UDSM and soon after when he joined CRDB.

    What happened?

    Upumzike kwa amani rafiki yangu.

    ReplyDelete
  12. Poleni sana Familia ya Mwema, alikuwa akifanya kazi na marehemu mama yangu mpendwa, mama baraka, pia alikuwa rafiki yangu pale tunapoonana. Mungu amlaze pema Mwema.
    Michael baraka Kiboga.

    ReplyDelete
  13. Pole kwa mke wa marehem,ndugu na jamaa na marafiki.rambirambi za USA zimewakilishwa na Pam,michango inaendelea,umoja ni silaha

    ReplyDelete
  14. Woh;i really shocked; jamani amekufa ameumwa nini? au ajali; i know him while at UDSM, he was doing BCOM while was doing ECONOMICS; rest in peace mwema;

    ReplyDelete
  15. Edwin, happened to be my friend for the first time when i was doing CASH transfer at CRDB Bank and from there, we shared A MOMENT of drinking wine and whisky every weekend at Rose Garden...he was a nice person and last two weeks everyday i have been having a BREAKFAST with him at CHEFS PRIDE....I AM SHOCKED WITH THE NEWS.

    BRO R.I.P

    You will always remembered by your friend

    Isaac Nguga Maguhwa

    ReplyDelete
  16. Nimesikitika mno. Huyu kijana alikuwa mshauri mzuri sana wa clients hasa pale ambapo anaona kuwa kama client akitaka kuingia biashara fulani na bank na akiona haitakuwa ya faida anakusahuri vilivyo. Sitakusahau, you did adviced me well. R.I.P mwema.

    ReplyDelete
  17. Poleni wafiwa. Ama kweli maisha ya dunia hii ni ya mpito. So young and so bright...RIP.

    ReplyDelete
  18. RIP Brother Edwin, Maisha ya binadamu kweli ni kama Mshumaa tu!imenishtua mnoo hii habari.

    ReplyDelete
  19. ooh no!so sad! huwezi amini michuzi nilikua naenda bank nasema ngoja nikamuulize mwema anisaidie issue yangu fasta nirudi job kitu kikaniambia embu soma michuzi b4 hujaondoka jamani si ndio nakutana na picha ya mwema eti ni marehemu...??? nimeumia kweli !MAY YOUR SOUL REST IN PEACE MWEMA...AMEN

    ReplyDelete
  20. Aisee wala siamini,kijana alikuwa so charming,helpfull jamani.RIP Mwema

    Melanie.

    ReplyDelete
  21. Nimepata taarifa hii kwa mshtuko mkubwa sana! nimemfahamu Mwema tangu Mlimani na pale CRDB alikuwa mtu wa msaada mkubwa sana! mwenyezi mungu amweke Mwema mahali pema peponi Ameni

    ReplyDelete
  22. Poleni sana,namkumbuka marehem kwani alinisaidia kupata bank statement ambayo iliniwezesha kwenda ughahibuni.Inasikitishwa kwa kuondokewa na vijana wadogo.ni kitu gani?????

    ReplyDelete
  23. whaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaat??????????????????? Oh my gosh...im out of words...eh MOLA IWEKE ROHO YA MAREHEMU MWEMA MAHALI PEMA PEOPNI AMEN!
    jamani what happened?siamini kabisa nimeshtuka sana

    ReplyDelete
  24. Mwenyezi Mungu Ailaze Roho Yako Mahala Pema Peponi Ndg Mwema. Kifo Chako Cha Ghafla Kimetushtua sana.

    ReplyDelete
  25. Jamanii nimeshtuka sanaa,he was very charming,helpfull,kind and ready to assist you..One of the best employees in azikiwa branch before he gt transfered to kariakoo... Will miss you..RIP mwema

    ReplyDelete
  26. Sina La kusema mumgu altwaa na Mungu kamchukua mwanae mpendwa tukae tukijua sisi ni wasafiri tu Mungu amlaze mahali pema peponi Amina

    ReplyDelete
  27. Bro Magesa was a very nice bro ever!! He was so cool, kind, helpful, charming. Im short of words to describe him. He was so caring indeed. He never lived in Dodoma area C, he spent his childhood in Tanga when his dad was working as a general manager of mkonge estates. In 1996 went to India for a heart surgery and he died few days ago from heart attack. May his soul rest in eternal peace!!!

    ReplyDelete
  28. Kakangu pumzika kwa amani kakangu umetuacha familia tunalia kila siku mpendwa wetu. Hakuna maneno mazuri ya kutufariji hapa duniani bali uwepo wako kwetu kama familia ulikua ni muhimu zaidi. Lakini kuondoka kwa mwanadamu katika hii dunia ni lazima ili litimie neno lake "Hakika mwanadamu aliezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi ni chache nazo zimejaa taabu na mateso.

    Unakumbukwa na wanafamilia kwa ujumla. pumzika kwa amani. Jina la Bwana libarikiwe. Raha ya Milele umpe eeh Bwana na Mwanga wa Milele umwangazie apumzike kwa amani.
    Amen.

    Pamela Mwema

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...