Hayati Emilian Mwidunda


Umoja wa wanafunzi wa kitanzania (UWATA) wanaosoma katika chuo kikuu cha urafiki-Lumumba nchini urusi unapenda kuungana na watanzania wote katika kumkumbuka dada yetu mpendwa EMILIANA MWIDUNDA aliyetutoka mnamo tarehe 16/11/2009.

UWATA kwa pamoja unapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki wote wa Mpedwa wetu huyo kwa ushirikiano wao wa dhati katika sala na maombi yao kwa kipindi hicho chote .

Kwa kuwa tunaamini kuwa kwake Mwenyezi Mungu tumetoka, na kwake ni marejeo tunaomba Mwenyezi Mungu aiweke roho ya dada yetu mpendwa mahala pema peponi.

“BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA…
JINA LAKE LIHIMIDIWE”
- AMIN.

Tangazo hili limetolewa na Uongozi wa Wanafunzi wa Kitanzania (UWATA),
Chuo Kikuu Cha Urafiki - LUMUMBA,
Moscow, Urusi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. tutakukumbuka daima dada yetu mpendwa,tulikupenda lakini mungu alikupenda zaidi,pumzika pema huko uliko!!

    ReplyDelete
  2. If roses grow in Heaven, Lord
    Please pick a bunch for me.
    Place them in my Emiliana's arms
    And tell her they're from me.

    Tell her I love her and miss her,
    And when she turns to smile,
    Place a kiss upon her cheek
    And hold her for a while......
    ...RIP Emmy....

    ReplyDelete
  3. Raha ya milele umpe Ee Bwana na mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani. Amina
    Mama Clara

    ReplyDelete
  4. Rest in Peace Emmy.stl remembaring the days we were in school together.

    Ex-Marian Girls High School student.

    ReplyDelete
  5. Yaaani imeniuma sana leo baada ya kugundua emmiliana kuwa hatupo nae tena ametangulia mbele ya haki.Thank you so much kwa walio weka hii kumbukumbu kwani wametusaidia hata sisi ambao tulikuwa hatujui,tumefahamu.
    Raha ya milele umpe Ee Bwana na mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani. Amina

    ReplyDelete
  6. So soon so Young RIP

    Mdau N.A

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...