Mchezaji wa Laxim Darts Club Issa akifanya vitu vyake
Maveterani wa mchezo G. Mwakalundwa na Mbegalo nao walikuwepo.
Mjomba Juma wa Laxim Darts Club akijitahidi kujinusuru na kipigo bila mafanikio
Picha ya pamoja ya wachezaji wa Police Mbeya na
Laxim Darts Club ya Tukuyu mara baada ya mtanange.
Mchezaji pekee wa Kike toka Central Police Darts Club
Bi. Mwakabwanga akitafuta malengo.

Njomba Michuzi, aslaaam aleikhum.
Pole sana na kazi ya zaidi ya miezi miwili ya kutuhabarisha mambo ya Uchaguzi Mkuu Tanzania Bara na Visiwani, kwa kweli nilikupata uzuri sana katika Blog ya Jamii. HONGERA SANA.

Hapa Tukuyu mambo safi sana, japo hali ya hewa bado sio nzuri, vumbi na jua kali nadhani ni yale yale ya Climate Change na ma-Global warming.

Jana Jumamosi kulikuwa na mchezo wa kirafiki baina ya Central Police Mbeya Darts Club na Laxim Darts Club ya hapa Tukuyu (Wanyambala), mchezo uliofanyika katika Bwalo la Polisi Mbeya Mjini.

Maafande wa Kituo Cha Kati waliwafanyia kufuru wanyambala wa Tukuyu kwa kuwagalagaza bila ya huruma kwa kuwafunga michezo 22 na point 6 zidi ya michezo 8 na point 3 kama inavyooneshwa katika score board:Nyota wa mchezo wa jana alikuwa Afande Kabeto ambaye alimburuza Mjomba Juma wa Tukuyu bila ya huruma 2-0 kwa round chache kuliko wote waliocheza na kushinda.
Katika hotuba yake ya ufunguzi, OCD Kituo cha kati Afande Silvester aliwakaribisha na kuwashukuru Laxim Darts kwa kukubali kuja na kushiriki katika mchezo huo, na kusisitiza kuwa jambo hili ni la kukuza mahusiano na ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na raia, na kwa kufanya hivyo tutaendeleza na kukuza dhana ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi kwani swala la ulizi na usalama ni la kila Mtanzania na hasa raia wema.

Aidha mwenyekiti wa Laxim darts Club (Wanyambala) Charles Mwakatobe alipotakiwa kutoa neno la shukrani, aliwashukuru Polisi Kituo cha Kati Darts Club kwa mapokezi mazuri na jitihada zinazofanywa hasa na OCD Silvester katika kuliweka Jeshi letu la Polisi karibu na Raia kwa kujenga mahusiano mazuri baina yao.

Leo Jumapili kutakuwa na kikao cha wadau wote wa Darts Mkoa Mbeya kitakachofanyika katika Bwalo la Polisi Mbeya ili kupanga ratiba ya mashindano ya Kitaifa ya darts. Wote mnakaribishwa.

Habari hii na
Ankal Juma wa Globu ya Jamii, Tukuyu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mukubilwe ba ku Tukuju! Ndaga nu kutoligwa!Wenzenu kulenga shabaha ni sehemu ya kazi za kila siku. Nyie wengine eti mpaka mtoke ofisini kushika kalamu na kubofya vitufe vya ngamizi ndiyo mfanye mazoezi ya shabaha!Ilikuwa lazima mufungwe tu!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...