


Na Ripota wetu.
BENKI ya FBME tawi la Dar es salaam leo imetoa msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha watoto wanaishi katika mazingira magumu pamoja na yatima kilichopo mjini Kigoma.
Akiongea wakati wa makabidhiano ya msaada huo Afisa mkuu wa huduma kwa wateja wa benki hiyo Jovita Francis alisema imekuwa ni kawaida kwa benki hiyo kila ifikapo mwishoni mwa mwaka kutoa misaada katika vituo vya watoto yatima ikiwa na moja ya huduma ya benki kwa jamii.
Msaada huo wenye thamani ya laki 5 ni mgawanyiko wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula kama mchele, unga , sukari , mafuta ya kupikia sabuni za kufulia na kuogea pamoja na mafuta ya kupakaa vilipokelewa na sista Rita Jose kiongozi wa vituo vya kulea watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima katika kanisa katoliki kurasini jijini Dar es salaam kwa niaba ya kituo cha watoto yatima sanganyigwa B kilichopo mjini kigoma .
Akitoa shukrani kwa niaba ya kituo hicho, Sista Rita Jose aliwataka watanzania wenye uwezo wa kuwasaidia watoto hao kwa namna yoyote ile kufanya hivyo kwani ni njia moja wapo ya kuonyesha hisia za upendo kwa watoto hao ambao maisha yao yanategemea misaada zaidi.
BENKI ya FBME tawi la Dar es salaam leo imetoa msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha watoto wanaishi katika mazingira magumu pamoja na yatima kilichopo mjini Kigoma.
Akiongea wakati wa makabidhiano ya msaada huo Afisa mkuu wa huduma kwa wateja wa benki hiyo Jovita Francis alisema imekuwa ni kawaida kwa benki hiyo kila ifikapo mwishoni mwa mwaka kutoa misaada katika vituo vya watoto yatima ikiwa na moja ya huduma ya benki kwa jamii.
Msaada huo wenye thamani ya laki 5 ni mgawanyiko wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula kama mchele, unga , sukari , mafuta ya kupikia sabuni za kufulia na kuogea pamoja na mafuta ya kupakaa vilipokelewa na sista Rita Jose kiongozi wa vituo vya kulea watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima katika kanisa katoliki kurasini jijini Dar es salaam kwa niaba ya kituo cha watoto yatima sanganyigwa B kilichopo mjini kigoma .
Akitoa shukrani kwa niaba ya kituo hicho, Sista Rita Jose aliwataka watanzania wenye uwezo wa kuwasaidia watoto hao kwa namna yoyote ile kufanya hivyo kwani ni njia moja wapo ya kuonyesha hisia za upendo kwa watoto hao ambao maisha yao yanategemea misaada zaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...