Mgeni rasmi kwenye hafla ya kuchangisha pesa za mpango wa Somesha Mtoto wa Kike (SOMKI) inayoandaliwa kila mwaka na Unity of Women Friends (UWF) Mama Margaret Chacha, Mkurugenzi mkuu wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), akitoa hotuba wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Kibo hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar usiku wa kuamkia leo
Mama Margaret Chacha akizindua
tovuti ya UWF kwenye hafla hiyo
Mshereheshaji Baby Kabaya akitangaza kwamba jumla ya shilingi milioni 47 zimepatikana katika hafla hiyo ya hisani ya SOMKI
Mama Margaret Chacha akitangaza washindi
wa bahati nasibu iliyochezeshwa
Baadhi ya wadau waliohudhuria hafla hiyo
wadau mbalimbali kwenye hafla hiyo
Meza ya kampuni ya mafuta ya TOTAL ilisheheni vilivyo
Mnunuzi wa picha ya mtoto wa kimasai (mwenye buluu) akikabidhiwa mzigo wale alioununua kwa dola za kimarekani 1,500 katika mnada uliopitishwa kwenye hafla hiyo
Mshindi wa simu ya Nokia na muda wa maongezi wa shilingi 50,000 akikabidhiwa zawadi yake baada ya kushinda bahati nasibu
Mdau akifurahia zawadi ya blender toka Mini Argos aliyoshinda kwenye bahati nasibu
Mama Chacha akiwa na wana UWF baada ya kuzindua tovuti yao
Meza kuu pamoja na wanachama wa UWF na waume zao. Walioketi toka kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Mh. William Ngereja, akifuatiwa na Gavana wa Benki Kuu Profesa Benno Ndullu na mgeni rasmi Mama Margaret Chacha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. watoto wetu wa kiume hakuna kusoma kuanzia mwakani loh, nami naanzisha ya kwangu somesha mtoto wa kiume kwanza, sawa?

    ReplyDelete
  2. Nimependa hii kweli ilikuwa hafla ya somesha mtoto wa kike hata kwa idadi kubwa ya akina mama wanao onekana hapa wamevaa ki kike hasa wale wanawake wa kitanzanai tunao wajuwa wameachana na vibody suti vya kiulaya ulaya wanapendeza kwa kweli na ilaeta maana kuwa na shughuli ya akina mama maana vile visuti wakati mwengine vinawatowa kwenye line big up mama zetu mkiwa hivi tunawaunga mkono kwa saana tu

    ReplyDelete
  3. Nadhani Jina sahihi la Mshereheshaji ni Baby Kabaya aliyekuwa mtangazaji wa East Africa Radio na sio Baby Madaha yule mwanamuziki wa Bongo Star Search.

    ReplyDelete
  4. wa kiume inabidi waendelee kuwa wajinga.?

    ReplyDelete
  5. mdau wa kwanza sio unavyodhani, sisi wabongo tunataka wakina-mama wapate uhuru wao kama vile mola alivyodhamiria. nikitazama hafla hii naona tuko mbele sana kulinganisha na nchi kama vile s/arabia,somalia,afghanistan,pakistan nk anyway we dont worry about them/sisi tunasonga-mbele tunaanza kubishana kuhusu mambo muhimu kama vile katiba mpya,uchaguzi halali nk Tanzania-Tanzania nakupenda kwa moyo wote!!!! msomali wa dom

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...