assalam aleykum?kaka Michuzi.

natumaini inshallah umzima wa afya,mimi ni mfurukutwa wa blog yetu ya jamii kwa mara ya kwanza nakuomba kajisehemu kidogo unitolee kwikwi yangu ambayo roho inaniuma sana mimi na wakazi wenzangu wa yombo kwa mfuga ndege na mwisho wa lami kuhusu mgao wa umeme unaondelea kila siku kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 12 jioni au ukipata umeme mchana usiku hupati .

ikiwa tulishatangaziwa kua mgao umeisha na maji yamejaa vilevile mitambo iliokua imeharibika imepona sasa sijui huyu mkataji umeme hana taarifa hizo.

kinachouma zaidi ni baadhi ya vitongoji vingine vinapata umeme bila matatizo.

Tunamuomba muhusika alifatilie swala hili wasiache watu wachache amabo wanaharibu jina la la shirika.mwisho tunaomba uongozi uliangalie swala hili.

Ahsante
wananchi yombo vituka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. ujue watu wengine wanahujumu kwa ajili ya kuendeleza biasha ra zao kama mafuta ya Taa, mishumaa na Majenereta.

    ReplyDelete
  2. AAA NA WEWE MTU WA YOMBO NI BORA UNYAMAZE TU WEWE HUJUWI KUWA WILAYA YA TEMEKE NDIYO WILAYA NASIKINI KULIKO ZOTE KATIKA MKOA WETU WA DAR ES SALAAM? NGOJA KWANZA WATOSHELEZWE WA OYSTERBAY, MASAKI, MBEZI BEACH,MIKOCHENI NA NYIE HUKO BAADAE BWANA NADHANI UMEELEWA SI NDIYO?

    ReplyDelete
  3. Duh..wewe Nina Kida hufai kabisa...ni kweli bwana...huku Mbezi Beach unakatwa kwa Ku-beep tu.....hivi kwani mgao kama mgao wa umeme bado upo?

    ReplyDelete
  4. Kwa kweli hii kata umeme linatuumiza sana wakazi wa yombo vituka, tunakatiwa umeme 12hours asubuhi mpaka kwenye saa 2 usiku. kila siku, na tulishaambiwa kuwa mgao umekwisha tena kwenye vyombo vya habari.Maeneo mengine walishasahau mgao.tunaomba tuambiwe tatizo ni nini.tufikishia ujumbe huu kwa wahusika, Asante sana

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...