Didier Drogba akiwa na wanamuziki waliotumbuiza katika mnuso huo
Didier Drogba na Fally Ipupa (shoto) na wageni kwenye mnuso

Mayenu kwa kwenda mbele
Fally Ipupa akionesha jinsi yenu linavyopigwa
Mshambuliaji wa Chelsea na Ivory Coast Didier Drogba akikaribisha wageni kwenye mnuso wa harambee ulioandaliwa majuzi na mfuko wake wa The Didier Drogba Foundation kwenye hoteli ya Grosvenor House jijini London Majuzi ambapo jumla ya pauni 500,000 za Uingereza zilipatikana kwa ajili ya ujenzi wa hospitali huko Abidjan. Nyota kibao wa soka na muziki walihudhuria, bila kusahau Globu ya Jamii iliyochanganyika na vyombo vingine vya habari kuripoti tukio hilo
Juu na chini ni baadhi ya vitu vilivyopigwa
mnada kwenye mnuso huo wa nguvu Jezi na picha za watu maarufu vilipigwa mnada
Akon, Drogba na wadau wengine wakilisakata rhumba
Ashley Cole na Michael Essien wakiwa na wadau. Wa pili kulia ni mdau Yasmin toka bongo
Fally Ipupa akiwachezesha sebene Drogba na wenzie
Mnuso ulifana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Mwinyi Wa Mikanjuni, TangaDecember 06, 2010

    Mrisho Ngassa, Henry Joseph, Mgosi, Redondo, Kijusso, Yondani na wengineo wote, igeni mifano mizuri hiyo na sisi wadau tuko nyuma yenu. Si lazima iwe kujenga hospitali, hata kusaidia dawa au chaki za shule tu ni mchango mkubwa tunaotegemea kutoka kwenu.

    ReplyDelete
  2. Siasa ndio inaponichosha Drogba ana changia kujenga hospitali kwao Wanasiasa wanagombania madaraka. Africa has along way to go.

    ReplyDelete
  3. Naona akina Ashley Cole wamevamia kuku wa kienyeji....no wonder Chelsea inayumba.....wangeuliza kwanini wachezaji wa mikoani wakija Dar wanacheza msimu mmoja tu halafu kwisha kazi.

    ReplyDelete
  4. safi sana drogba,wachezaji wetu igeni mifano hii,sio mnawazia ndumu tu na vimwana vya ilala na k.koo.

    ReplyDelete
  5. Natoka nje ya mada jamani mbona hamkusema tulivyopata kipigo cha mbwa mwizi kutoka kwa west ham? mie ni man u damu ila nimeshtuka lo! kweli walitu over do doze grrrrrrrr!!!! tukirudi kwenye mada hakika shughuli ilifana sana icha tu zinasema hivyo.

    ReplyDelete
  6. we anony wa tatu umeniacha hoi!ha ha haa...suupuu ya kuku wa kienyejii...wapi banza??

    ReplyDelete
  7. hahahahaaa umenivunja mbavu zangu, kuku wa kienyeji ndio wanawake wa bongo au, umenifanya nicheke mpaka sina hamu. ama kweli ukistaajabu ya musa utaona ya filauni

    ReplyDelete
  8. Eti igeni Mfano, hivi hawa wachezaji wa TZ wanalipwa kiasi gani zaidi ya watanzania wengine?. Utamlinganishaje Mrisho Ngasa na Drogba amaye nalipwa hela nyingi ambazo nyingine zinaweza kuw ani za starehe?

    Mrisho ngasa anamatatizo kibao yake binafsi hayajamaliza tokana na malipo anayo pewa nalafu unataka kumlinganisha na Drogba ambaye mshahara wa week moja tuu unamaliza matatizo ya uko wake wote.

    Msitake kuonea wasanii na wanamichezo wa Tanzania lazima mtu ujisaidie kwanza ndio usaidie wengine ,Kipato wanachopata sio kingi kiasi kiwepo cha kuongeza kusaidia wengine.

    Jiulize wewe unaye andika hapa ambaye labda una mshahara unalingana na huyo Mrisho umesha fanya nini kusaidia wengine ,sio kukaa kulalamikia wachezaji sababu anatajwa jina sana wakati kipato chake labda hakitofautiani na chako.

    ReplyDelete
  9. kuna wadau wameniacha hoi sana hapo juu...wengine walikuwa hawajui maana ya " kuku wa kienyeji" hahahaaa any way ni kweli kipato ya wanasoka wa tanzania hata siku moja haitakuja kutokea kikafananishwa na wachezaji wa kulipwa wa ulaya, ni kweli mdau hapo juu amesema mshahara wa week moja tu wa drogba unaweza kutatua matatizo ya ukoo wake wote na pengine sio ukoo wake tu hata na kijiji chake chote!!!!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...