Balozi Massinda alikutana na Waziri Paris na ujumbe wake ambao walifika Ubalozini kuzungumzia tamasha la kuenzi mila na utamaduni wa Mwafrika litakalofanyika mnamo Septemba 2011 jijini Halifax, Nova Scotia.
Pamoja na maelezo kuhusu tamasha hilo, Waziri Paris alielezea jinsi mkutano wa "African Diaspora Heritage Trail" ambao ulifanyika nchini Tanzania mwaka 2009 ulivyotoa changamoto kwa watu wenye asili ya Afrika walioko ughaibuni kutambua umuhimu wa Afrika Mashariki kama chimbuko lao sawa na Afrika Magharibi.
Kwa hiyo wenyeji wa tamasha la Halifax wangependa Tanzania ishiriki na kuonyesha utamaduni na sanaa zake kwenye tamasha hilo. Waziri Paris aliomba Balozi Massinda asaidie kuhamasisha ushiriki wa Watanzania wanaoishi Canada pamoja na taasisi za Tanzania. Kwa upande wake Balozi Massinda aliahidi kuyafanyia kazi maombi hayo.
Aidha alishauri Waziri Paris na ujumbe wake wapange kuonana na Mabalozi wa nchi nyingine za Afrika Mashariki na kuwaalika nao washiriki kwenye tamasha la Halifax.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...