Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu na Bunge),William Lukuvi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar ofisini kwake kuhusiana na Tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Babu Mchungaji Ambilikile Mwasapila huko Loliondo.
Mh Lukuvi alibainisha kuwa serikali haina mpango wa kuzuia tena huduma hiyo kwa kuwa inahusisha imani za watu." Serikali haina mpango wa kuzuia huduma hiyo na badala yake imeunda kamati itakayofanya kazi kwa kushirikiana na mchungaji huyo ili kuhakikisha jamiit inapata huduma hiyo kwa utaritibu unaostahili"alisema Lukuvi.
Mh. Lukuvi alisema kuwa kamati hiyo inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambayo imeanza kazi jana imezuia magari yote yanayokwenda kijijini hapo ili kutoa nafasi kwa Mchungaji Mwasapila kuhudumia wagonjwa waliopo hadi idadi yao itakapopungua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. hii deal ya wakubwa. ynai hata serekali inaamini nguvu za giza !

    ReplyDelete
  2. Wewe Anon wa kwanza acha kuwa mkiritimba,Imani za watu unasemaje nguvu za Giza,kibaya kwako kizuri kwa mwenzio.wewe usipoweza kuamini waache wenye kuamini subiri yakukute utakwenda na wewe au ndugu zako wamefika kama ujafahamu.

    ReplyDelete
  3. WATANZANIA WENGINE UWEZO WA KUFIKIRIA NI ZIRO. INGEKUWA NI MZUNGU KATOKA MAREKANI NA HII TIBA NADHANI KUSINGEKUWA NA MIKANGANYIKO. WABONGO HATUKUBALI KABISA KUWA WATU WAPO WENYE IMANI, VIPAJI NA UWEZO KUZIDI WENGINE. WE UNAYEJIFICHA WA KWANZA ZAMU YAKO YAJA WEWE.

    ReplyDelete
  4. kaka pole kwa kazi pia nashukuru kwa kutuweka karibu na wenzetu, ilaq tu mimi maoni yangu ni kuhusu huu utaratibu wako wa maneno unapokuwa unaandika, unachanganya kiswahili mno, kwa mfano juma chama na my wife wake hiyo ni nini? au chuo kikuu cha ardhi university pia nini? kaka jaribu kuweka utaratibu mzuri wa kiswahili chetu, wewe ndiyo mkuza kiswahili chetu kaka mkubwa. kila la heri na kazi njema.............

    ReplyDelete
  5. Wee unayelalamika kiswahili kiswahili...Mbona hata lugha za kidhungu zina misema mingi tu mipya na inaingizwa kwenye dictrionary zao kila mwaka? Ina maana kiswahili chetu ndio hakikui tu ? kwa taarifa yako kiswahili unachoongea leo sio walichoongea baba zako...Lugha hutembea haisimami...

    Kwa kukusaidia tu Google new word & slag 2010 Merriam webster

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...