Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akizungumza wakati wa hafla ya kubadilishana hati ya Mkataba wa msaada wa Sh. bilioni 251. 62 kwa ajili ya kusaidia Sekta ya maji na Umeme nchini.kulia ni Mkurugenzi wa benki ya ‘Africa Development’ (AFDB),Gabriel Negatu.Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, akibadilishana hati ya Mkataba na Mkurugenzi wa benki ya ‘Africa Development’ (AFDB), Gabriel Negatu, ikiwa ni msaada wa Sh. bilioni 251. 62, kwa ajili ya kusaidia Sekta ya maji na Umeme.Hafla hiyo imefanyika kwenye Ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Picha na Vicent Tiganya-MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. duuu.ina maana msaada watu wanaandika mkataba.au mkopo??sijaelewa hapa.werevu wanisaidie.

    ReplyDelete
  2. Jamani chonde chonde, hizo hela tunawaomba zisaidie kufufua mitambo ya umeme nchini,tunakuomba sana Waziri simamia vizuri jambo hilo. Tanzania inatia aibu jinsi Jenereta zinavyopiga kelele nchi nzima.Nchi za wenzetu ulaya umeme na maji vikikatika hata kwa dakika mbili tu ni kosa la jinai. Uliza Marekani.

    ReplyDelete
  3. cha ajabu tunaambiwagwa zikitolewa tu, zinafanya nini?nayo tuambiwe na uthibitisho

    ReplyDelete
  4. kitu cha kwanza napenda kujua huo ni MSAADA ama ni MKOPO??? na kama ni MKOPO hakuna haja ya kuandika kuwa ni msaada mana msaada haulipwi. thanks anyway from Bank of Africa. pili, Serikali ilikuwa inahitaji Tsh billion 300 kutatua matatizo ya umeme, haya hiyo 250 waongezee hapo kidogo waanze kusolve tatizo. mana hali si shwari.

    ReplyDelete
  5. NIjuavyo mimi bank huwa zinatoa mikopo.nadhani huu WALIOPEWA TZ,NI MASHARTI NAFUU.KULIPA NCHI IKIWA TAJIRI MIAKA 50 IJAYO.tatizo riba yake.lol

    ReplyDelete
  6. HUU "MKOPO" AU KWA LUGHA NYINGINE YA "WEREVU" (MSAADA)NI KATI YA MINGI TUNAYOIONA NA KUSIKIA KATIKA VYOMBO VYA HABARI. NCHI INATAFUTA MAENDELEO BILA YA [ENERGY PRODUCTION]. NAFIKIRI NI SISI TU DUNIANI TUNAOFUATA MFUMO WA UWEKEZAJI BILA YA KUWA NA NGUVU YA UMEME NA MAWASILIANO [MAZINGIRA MAZURI KWA WAWEKEZAJI].KWAKIFUPI NI KWAMBA TUJIANDAE "KUOMBA KUSAMEHEWA MADENI KUANZIA LEO"

    ReplyDelete
  7. KAZI YA BANK NI KUTOA MIKOPO YA FEDHA AMBAZO LAZIMA ZIRUDISHWE KWA RIBA NONO NDANI YA KIPINDI KIFUPI NA SI KUTOA MSAADA KAMA WEWE UNAVYOTUDANGANYA HAKUNA MSAADA WATU WANASAINI MKATABA

    ReplyDelete
  8. Mungu mkubwa sasa umeme utawaka, au sababu itakuwa nini tena, giza limeonekana hata bank ya africa! Wenye madaraka waache ulaji ili tuendelee, maana tukiwa na maendeleo hata ukila havionekani, kazi kwenu

    ReplyDelete
  9. Tanzania bila umeme, inawezekana. Mbona tunadunda hatujafa. Kuna watu toka wazaliwe hawajawahi ishi nyumba yenye umeme. Only 10 % ndo tuna umeme na bado government inashindwa kutuhudumia. Choka mie.

    ReplyDelete
  10. We wiil go shopping now, Mkulima haoni ndani hii pesa ni ya watu wa mjini tu. Nani alikuambia kuna mpango wa umeme, Tanesco hawataki hata kuhakikisha wanatowa umeme kwa watu hata kama upo na hakuna mgao, wameshindwa hata kukusanya pesa kiuhalali, mmoja nakuambi lipa milioni 10 mwingine ankuambi nipe laki tano mfukoni na utalipa milioni mbili tu, Wafanyakazi wao ndiyo wezi wakubwa wa umeme. Sasa nyie mtabweteka weee kumbe shirika limeoza. Ache aje mchina atudanganye tena achukuwe pesa yote iende china, kwani atahakikisha kila nyumba inapata umeme na ankusanya pesa kwa nguvu zote. Yani sisi waafrika akili zetu siji=ui zipo wapi? kwa nini hatuwezi kazi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...