Wachezaji wa kutumainiwa wa Laxmi Darts Club,
kuanzia kulia ni Mawazo, Neema na Ezekia
Timu nzima ya Laxmi Darts Club wakiwa wametinga na uzi mpya

Habari Mjomba Issa,

Kwa majonzi tunaungana na Wasanii, washereheshaji , wana burudani na Watanzania wote kwa ujumla kuomboleza kifo cha wasanii wa Five Stars Modern Taarab, aidha tunawatakia wapone haraka majeruhi wa ajali mbaya iliyotokea. Poleni sana na wote tunawatakia subira – “Innah lau maswabilinakila mwenye kusubiri yupo karibu na mwenyezi mungu


Mjomba jana 22/03/2011 ilikuwa ni siku ya heri sana kwa wanachama na wapenzi wa Laxmi Darts Club kwa kukabidhiwa jezi bin uzi toka kwa wafadhili hapa Tukuyu (Champion) na pia Darts Board na Mishale toka kwa mfadhili wa Dar-es-salaam ambaye hakutaka kutaja jina lake wala thamani ya vifaa hivyo.


Hii yote ni kutokana na wewe mjomba kuandika habari zetu katika Globu ya Jamii na watu kujitokeza kutusaidia, hivyo shukurani za pekee ni kwako Mjomba Issa Michuzi kwa kututangaza. Ni imani yetu kuwa wengi wataendelea kutupa sapoti wanyambala wa Tukuyu katika vifaa. Shukurani wote.


Mwisho ni swali kwa wenye taarifa juu ya Club maarufu hapo Dar Kishamapendo Darts Club (Club Kongwe) ya pale Ilala je bado ipo? tupeni contacts zao tuje kukipiga wakati wa Pasaka.


Habari na picha

Mjomba Juma wa Globu ya Jamii, Tukuyu

Kwa mawasiliano: laxmidarts.club@gmail.com

Katibu, Mwakatobe 0787 087 955

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...