Msanii mkongwe wa tasnia ya filamu Bi Christina Innocent a.k.a Mama Bishanga akiwa na mai hazbendi wake Bw. Marolen wakati wa kumeremeta hivi karibuni katika kanisa la St. Peters jijini Dar. Bw Harusi anatokea Limpopo, Sauzi. Hivi sasa wako Columbus, Ohio, Marekani ambako ndiko wanaishi
Ni wakati wa kukata keki kwenye mnuso hoteli ya Peacock jijini Dar
Bi Harusi akiingia Peacock hotel kwenye ukumbi kwa mila za Wamakua wanawake hulala chini na bibi harusi kupita juu yao mpaka kwenye kiti atapokaa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 20 mpaka sasa

  1. Michuzi sasa bibi harusi hukanyaga sehemu gani ya kiwiliwili baada ya binadamu huyo kulala chini? hii mpya! nyumbani kweli tambarare

    ReplyDelete
  2. Hii ni jump the women, not jump the broom!!!!! ha ha ha mila na utamaduni oyee.

    ReplyDelete
  3. Duh.........mi sikubali, siwanaumia sana hao waliolala hapo...mbaya zaidi kiatu chenyewe cha mchuchumio..!!! halafu mwenyewe bongeeeeeeeeeee!
    Kapendeza sala.

    ReplyDelete
  4. Kudumisha mila hii ni muhimu, lakini inapokuwa bibi harusi ana mwili mkubwa na mzito kama ulivyo huo wa bibi harusi huyo na kisha kavaa viatu vyenye visigino vyenye chongo si inakuwa hatari kwa hao wanaokanyagwa, maana upo uwezekano wa wao kuumizwa na viatu hivyo?. Afadhali bibi harusi eidha angevua viatu au angevaa viatu vilivyo flat ambavyo visigino vyake havina chongo.

    ReplyDelete
  5. Am happy for her,
    Yaan ndoa ni ndoa hata kama ni mtu mzima jamani.

    ReplyDelete
  6. hii harusi mbona watu wenyewe wanaonekana umri umekwenda ni harusi au ndoa? na hii ya kukanyaga wenzie wakati wamelala chini ni kali ya aina yake halafu naomba kuuliza huyu bi shanga ni yule wa zamani aliyeigiza na dr cheni kama wife wake akaekti kama kilema wa mguu mmoja? naomba wanaomjua zaidi wanijuze pls

    ReplyDelete
  7. Mangi wa KiboshoApril 29, 2011

    Mama Bishanga Hiki Kibabu cha watu umekiibua wapi?

    ReplyDelete
  8. Ndoa ya uzeeni HONGERA

    ReplyDelete
  9. Hongera Dada Christina! Kweli ulimeremeta!

    ReplyDelete
  10. karibu COLUMBUS

    ReplyDelete
  11. Ndoa za uzee nyie ni nani kumpangia mtu muda wa kuoa au kuolewa. Tradition zenu mkae nazo huko huko. Hawa wanaelewa wanachokifanya nyie mnaoona wazee sijui mliolewa na miaka 22 na kuoa na mika 25 look at you now...Unakalia kuangalia harusi za wenzenu kwa vijicho kwa vile hukuenjoy harusi yako au you are in a very miserable marriage kwa vile ulirush bila kujua mtu unayemoa au kuoa.

    Mtu anayejua maana ya harusi sijui ndoa hiyo ni kwa wa bongo the union is the union ndugu zangu no matter what ..Nyie mliokalia hiyo ni ndoa basi kwa taarifa yenu kama ni hivyo kila mtu anayeoa/kuolewa sasa hivi ni ndoa tu no matter the age...Prince William na Kate walikaa pamoja kabla ya harusi yao leo mbona hamjafungua mdomo kusema hiyo ni ndoa na sio harusi? Acheni kusema sema kwa vile mko under hii anonymous umbrella lakini ujue hata kama hakuna anayekujua lakini unajijua mwenyewew jinsi low life na low mind uliyonayo. Wanasema watu waliodepress ndio wanakwenda kwenye blogs na kuandika vitu (negatives) kwa watu wala hawawajui halafu wanajisikia vizuri. Lakini in real life wamelost na hizo comments zinareflect maisha yao...i.e huyo/hao waliocomment hapo juu wanaweza
    a) hawajaoa/kuolewa pia na wanajiona wamepita ule umri wa TZ tradition kuolewa sasa wanamwonea wivu mwenzao kapata mume at that age...Wanajiuliza why her or why him
    b) Hawana boyfriends/girlfriends sasa wanamwonea wivu mwenzao kapata.
    c) wameshaoa/ kuolewa lakini hawakufanyiwa harusi waliyoipenda sasa wakiona za wenzao roho inauma wanatafuta sababu ya kukosoa ili waone wamelingana

    Hivyo kabla hujahit that send button read your negative comment again ...utaona inakureflect your low life.

    kaolewa kaolewa alikompata mumewake nyie inawahusu nini? Why don't you just say congratulations...Yaani blog za wabongo ndio zina negative minded people ukipitia blog za nchi zingine yaaniutaona jinsi wanavyofurahia tukio la mtu . Hata hawamjui...na ujue roho ya korosho haiendelei.

    ReplyDelete
  12. Mama Bishanga, HONGERA SANA SANA. Umependeza mno and i want to wish you all the Best in your future. Naomba kama naweza kupata contact zako za Ohio nikutafute, unaweza kuwa umenisahau but ulinisaidia sana sana ulipokuwa South Africa and i would realy like to talk to you again au hata nikuone.
    Again umependeza, you look young and beautiful

    ReplyDelete
  13. Safi sana na hizi ndoa za utu uzima nazipenda sana, they know what they want and they will absolutely enjoy every bit of their life.

    Hongera.

    ReplyDelete
  14. waftni haooooooooooo kibabu umekitoa wapi?? inakuhusu nn? eti wazeee? kwani wazee ndo wanatakiwa kuishi bila mume? au mke?. Acheni kupangia watu maisha bwana. HONGERENI SANA MAHARUSI....Mama bishanga big up kupata mwenza. Im happy 4 u!

    ReplyDelete
  15. Ndoa ya Prince Wills na Kate haina utamu maana tayari wameshaonjana!! Ughaibuni kuna mila ya "bachelor's party" hii huwa mtarajiwa huwa anafanya ngono siku kadha kabla ya ndoa kwa watu wengine mpaka achoke!!

    ReplyDelete
  16. Ukweli siku zote unauma sasa nyinyi mnaopinga kwani huyu sio BABU?

    ReplyDelete
  17. hahaha,why are u bitter?(anony of 5.24am).. its called opinion and not everybody got the same..So long you put your pics in public, expect some scrutiny whether u like it or not! Take a chill pill and let people write what they want to.

    ReplyDelete
  18. Jamani babu yupo Loliondo,huyu siyo babu.

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 02, 2011

    Jamani kumbe babu wa Loliondo alikuwa hajaowa?wamependeza sanaa.

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 02, 2011

    BABU WA LOLIONDO MBONA KIJANA?HONGERENI SANA,NAWATAKIA MAISHA MEMA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...