Mshindi wa kwanza wa taji la Vodacom Miss Dar City Center Alexia William akiwa kwenye picha ya pamoja na mshindi wa pili Salha Israel (Kushoto) na mshindi wa tatu Jenifer Kalokola mara baada ya kutangazwa washindi. Shindano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki jijini Dares salaam.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Slaa akimkabidhi mshindi wa kwanza wa taji la Vodacom Miss Dar City Center Alexia William zawadi ya shilingi Milioni 1/- zilizotolewa na waandaaji wa shindano hilo. Anayeshuhudia ni mke wa Meya Slaa, shindano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki jijini Dares salaam.
Vodacom Miss Dar City Center Alexia William akipunga mkono mara baada ya kutawazwa kuwa mlimbwende wa kanda hiyo. Wengine kutoka kulia kwake ni mshindi wa pili Salha Israel, wa pili kutoka kulia ni mshindi wa tatu Jenifer Kalokola, wa kwanza kutoka kushoto ni mshindi wa nne Maryvine Kenzia na kulia mshindi wa tano Lilian Paulo, shindano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki jijini Dares salaam.
Mkuu wa itifaki wa kamati ya Vodacom Miss Tanzania Albert Makoye, Mtaalam wa Masuala ya Habari wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu na Afisa Udhamini wa kampuni hiyo Ibrahim Kaude wakisoma ujumbe wenye jina la mshindi wa Miss University (UDSM) Chiaru Masonobo ili walitangaze kwenye shindano la Vodacom Miss Dar City Center lililofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Saalam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2011

    Hivi hizi nywele ni zao au ndo pendezesha tu! Hii tunadanganyana jamani Beauty is naturally in and out. mwekeni vile vile alivyo tumuone avae kikawaida bila ya kujirembesha, yaani kama katoka kijijini. Mtoto wa kimasai ni mzuri bila ya kuweka make up na nywele za kafa ulaya. Niiteni mshamba au sipendi maendeleo lakini mhhhhhh!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2011

    Aaaah chaurembo wa ukweli ni Flaviana matata tuu model wa ukweli no feki feki hair yeye na upara wake tuu wa kibantu na uback beauty wake na yuko bomba kichizi.. wazungu wanamkoma!
    mwanamke kujiamini bwana!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...