Tasnia ya muziki wa injili Tanzania  imezidi kukua na hatimaye kuzidi kufikia malengo yake ya kulitangaza neno la Mungu kupitia muziki. Hii imedhihirika wazi kutokana na kila kukicha kuibuka kwa watumishi wapya wenye vipaji machachali katika muziki huo.
Bertha Samwel













































Bertha  Samwel ni mmoja kati ya wanamuziki wapya wanaoibukia  kwa kasi katika muziki wa injili . Mwanadada huyo anatamba na wimbo unaokwenda kwa jina la “NISAIDIE BABA” akieleza kuwa anapenda kutenda mambo mema lakini anajikuta lile baya analolichukia ndilo analotenda kwahiyo anamuomba Mungu amsaidie na amuongoze kwa maana peke yake hawezi. Ama kwa hakika ukiusikiliza  wimbo huo  unagusa sana mioyo na maisha ya watu ya kila siku.

Bertha ambaye asili yake ni Kyela,mkoani  Mbeya ameanza kuimba muziki wa Injili tangu akiwa mtoto kipindi akihudhuria Sunday School huko Mbeya. Kwa sasa ni mwanachuo katika chuo cha Tumaini na anakaribia kukamilisha album yake ya kwanza ya muziki huo wa Injili ambayo bado hajaipa jina.

Anasema kuwa maneno yanayoimbwa na waimbaji wa muziki wa Injili ni mahubiri tosha, kwahivyo anawaomba mashabiki wa muziki huo wasikilize muziki wao kwa nia ya kupata habari njema za wokovu na si kuburudika tu kama baadhi yao wanavyofanya, “Ujue unaposikilizia muziki wa Injili utakuta kuna ujumbe fulani wa kiroho, ujumbe wa kuokoa na kubadilisha maisha ya mtu kwahivyo ninawasihi mashabiki ni vyema kusikiliza kwa umakini na kuyazingatia tunayoyaimba kwa maana ni ujumbe tosha ambao bwana anatupatia kupitia roho mtakatifu tuuimbe kuufikisha kwetu na kwao pia” alisema Bertha.

Hivi karibuni Bertha atazunguka kufanya maonyesho akimsindikiza mwanamuziki wa muziki wa Injili K BAZIL ambaye hapo awali alikua akiimba muziki wa Bongo fleva akitamba na wimbo wa RIZIKI aliowashirikisha Stara Thomas na Bizman katika uzinduzi wa album yake ya kwanza ya muziki wa Inili inayokwenda kwa jina la “YESU ANANIPENDA” .  Crispin Challe ambae ni Mkurugenzi Mtendaji wa Ufufuo Music & News Blog site (www.ufufuomusic.blogspot.com) ambao ndio waandaaji wa tamasha hilo amesema tamasha hilo litafanyika kwa mara ya kwanza katika mkoa wa Iringa siku ya Jumapili ya tarehe 5/06/2011 na baadae kuendelea kufanyika katika kila mkoa amabapo K BAZIL amewahi kufanya shoo akiwa kwenye muziki wa Bongo fleva kabla ya kuja kumalizikia Jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 30, 2011

    Safi sana Bertha, waambie hao wanaotafuta pesa ama kusikiliza kwa kuburudika, tumeona wengi wakiimba nyimbo za injili na wakizicheza kwa kama dansi la akudo lakini hawaangalii kilichoimbwa. Watu tusikilize ujumbe mungu akubariki

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...