

Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
kama ni kuuenzi umoja wa kitaifa basi katiba ishughulikie matatizo ya udini yanayotugawa. Iwepo sheria ya kuchunguza na kuadhibu wabaguzi kwa misingi ya dini makazini, sehemu za huduma kama sibitali, sehemu za sheria kama polisi na mahakamani, mashuleni n.k.
ReplyDeleteTusiache dhamana ya kukemea udini iwe mikononi mwa mabosi ambao wanaweza kuwa wadini na wazalendo wa dini zaidi kuliko taifa.
Dhamana ya kufuta udini iwe mikononi mwa dola kisheria/kikatiba.
Sidhani kwa hilo kama tutachafua amani bali kuikomaza. Tusipofanya hivyo basi mjuwe tunafuga wadini serikalini na sehemu nyengine za umma.
Watu hawapendi kuzungumzia tatizo la udini nalo linaendelea kumea mizizi na kuleta matunda machungu. Tuung'owe huu mti kisheria. Tukifumba macho, leo ni mimi kesho ni mwanao.
ReplyDeleteKukemea tuu kwa kulaani ubaguzi hakutoshi.
Nahisi hutajisikia vyema mwanao akimaliza shule akanyimwa ajira kwa misingi ya kidini au kikabila halafu hana namna wala sehemu ya kulalamika kisheria.
Ndiyo nchi hii inafuata utawala wa kisheria, lazima kila tatizo litatuliwe kisheria, hata ubaguzi.
ReplyDeleteKama inafikia watu kubadilisha majina ili kuepuka ubaguzi basi serikali imelala saana au ni lengo la baadhi ya wakuu serikalini kwa makusudi kisirisiri.
ReplyDeleteKatiba ya sasa inatakiwa kujibu hili ili watu woote wawe huru kukaa na majina yao bila kuadhibiwa kielimu, kijamii, kirafiki, kikazi, kisheria, kihuduma, kibiashara n.k.