Hii ni Video fupi ya Ziara iliyofanywa na Tanz UK ikiwakilishwa na mwenyekiti wake Dr John Lusingu alieambatana na Mkurugenzi wa Aset Asha Baraka. Ziara hii iifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwa dhumuni ya kutembelea kampuni ya Computer 4 Africa chini ya uongozi wa mwenyekiti Aseri Katanga ambayo inajishughulisha na ukusanyaji wa computer zilizotumika kutoka katika mashirika na taasisi mbalimbali hapa UK, kisha kuzisafisha, kuzikarabati na kuziongezea uhai mpya unaonendana sambamba na teknolojia mpya na mwishowe kuzisambaza Africa Nzima. Tanzania ni mojawapo ya nchi za kiafrika ambazo zimenufaika zaidi katika mpango huu kabambe ambapo shule zaidi ya mia zimenufaika kwa kupewa msaada huu.
Huu ni mmoja wa mifano mizuri ya kuigwa kwa watanzania wote hususani waishio ughaibuni/ Diaspora ili kusaidia kuleta maendeleo nchini kwetu na hatimaye barani afrika bila ya kutegemea serikali pekee.
Asanteni
URBAN PULSE CREATIVE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. NATEGAMEA WATANZANIA sasa watambue second hand VITU VILIVYOTUMIKA ULAYA VINA SOKO VILEVILE.Nimemsikia ASHA BARAKA na mwenyekiti wa watanzania akizungumza.
    Nina kaka yangu anauza vitu vya mitumba kama TV,FRIJI,PHOTOCOPY lakini anapata taabu sana kuwaelimisha wananchi wanasema haaaaa hivyo ni vitu chakavu bei kubwa sana na hata mtu anauwezo kidogo ukimwambia njoo kwenye duka langu la mitumba anasema hivyo ni vitu chakavu siji kununua na maneno mengi.
    Ndugu zangu tuwaelimishe hawa ndugu zetu wajue hata Ulaya kuna vitu vya second hand au mitumba vinauzwa kwa bei tena kubwa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...