Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohammed Shein
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Ali Mohammed Shein leo amemteua Fatma Gharib kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar.

Taarifa ya Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Abdulhamid Yahya Mzee amesema uteuzi huo umeanza rasmi kunzia leo Juni 15,2011.

Fatma Gharib Bilal aliwahi kuwa Mwalimu na kufanya kazi katika Wizara ya Fedha Zanzibar na kabla ya Uteuzi huo alikuwa akifanyakazi katika Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maswala ya Idadi ya Watu (UNFPA) Ofisi ya Zanzibar.

Ndugu Fatma Gharib Bilal ana shahada ya Uzamili katika Uchumi aliyoipata nchini Urusi.

Pia Dk Shein amemtaua Omar Khamis Juma kuwa Ofisa Mdhamini katika Wizara ya Katiba na Sheria Pemba.

Uteuzi wa Ofisi Mdhamini umeanza leo Juni 15,2011

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...