Afisa Viwango Mkuu wa Shirika la Viwango la Taifa (TBS) Obadiah Msaki akitoa mada kwa wafanyabiasha watakaonyesha bidhaa zao katika maonyesho ya 35 ya biashara ya kimataifa jijini Dar es salaam juu kuzingatia bidhaa zenye viwango katika maonyesho hayo.
 Mratibu wa kusimamia sheria za afya na mazingira Manispaa ya Temeke William Muhemu akitoa mada kwa wafanyabiasha watakaonyesha bidhaa zao katika maonyesho ya 35 ya biashara ya kimataifa Dar es salaam juu ya wajibu wa usalama wa vyakula na usafi wa mazingira katika maonyesho hayo yatakayoanza mwishoni mwa mwezi huu.
Baadhi ya wafanyabiashara watakaoshiriki maonyesho ya 35 ya biashara ya kimataifa Dar es salaam wakiwa katika semina elekezi ya maandalizi kabla ya kuanza kwa maonyesho ambayo yataanza rasmi tarehe 28 Juni mwaka huu. Jumla ya Nchi 17 zitashiriki maonyesho ya mwaka huu.picha na Tiganya Vincent, dar es salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 16, 2011

    Hii kali ,chumba cha mkutano wa wafanya biashara wa kimataifa hakina hadhi na ukizingatia joto la bongo!,lakini mkutano wa kuwaandaa warembo huwa unafanyika sehemu maarufu kama Bagamoyo au Kilimanjaro hotel nk.hata vikao vya harusi vinafanyika sehemu nzuri.
    tuzingatie umuhimu wa haya mambo jamani,tuna biashara nyingi za kuzitangaza kutoka Tanzania.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 16, 2011

    naungana na Annony wa kwanza, semina ya viwango inafanyika katika ukumbi ambao hauna VIWANGO....
    Tuwe makini jamani especially pale tunapofanya vitu vya ngazi ya kimataifa...

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 16, 2011

    Zimebaki wiki mbili tu kabla sabasaba kuanza, lakini Tovuti za Board of External Trade (BET) na ile TANTRADE Tanzania, ambazo zilipaswa ziwe active kutoa maelezo kuhusu sabasaba hii zimelala. Maofisa wapo maofisni wamejaa na kung'ang'ania kuendesha magari makubwa lakini kazi hawataki kufanya. Jamani amkeni, mnategemea maendeleo kwa mtindo huu????!!!! As of now, hakuna mahali popote unapoweza kupata taarifa zozote za uhakika kuhusu sabasaba hii, inakatisha tamaa kweli kweli, Mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...