![]() |
| Mkurugenzi wa ZIFF Profesa Martin Mhando akiongea na wanahabari akiwa meza kuu na wajumbe wa tamasha hilo hoteli ya Southern Sun jijini Dar |
MAANDALIZI Tamasha la 14 la kimataifa la filamu la Zanzibar International Film Festival Festival (ZIFF) sasa yamesha kamilika ambapo linatarajiwa kuanza mwishoni mwa wiki hii.
Akizungumza jana katika mkutano na waandishi wa habari Mkurugenzi wa ZIFF Profesa Martin Mhando amesema kwamba tamasha hilo la mwaka huu litakuwa la aina yake hasa kuzingatia uzoefu walionao tangu lilipoanzishwa.
Profesa Mhando alisema kuwa mwaka huu katika tamasha hilo kutakuwa na mambo mengi ya kuvutia ikiwa ni pamoja na maonyesho ya wanamuziki wenye majina na wa Kimataifa kama Shaggy na Oliver Mutukudzi.
Mbali ya wasanii hao pia filamu 71 zitaonyeshwa ikiwamo filamu za hapa nchini. Mhando alisema kutakuwa na filamu za mataufa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoka nchi za Iran movie, Swahili Bongo day na filami nyingine kutoka katika nchi mbalimbali zitaonyeshwa.
Wakati huohuo Mhando ameongeza kuwa kuwa filamu 58 zitashindanishwa na zawadi mbalimbali zitatolewa. Pia amesema kuwa katika tamasha hilo watatoa tuzo ya heshima kwa marehemu Hammie Rajab ambaye alikuwa mtengetezaji wa filamu mzoevu hapa nchini aliyefariki dunia Aprili 21 mwaka huu.
Mbali ya kuwa mtengenezaji wa filamu Marehemu Hammie pia alikuwa mwandishi wa vitabu vya tamthilia pia aliwahi kufanya kazi mbalimbali za uandishi.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...