Balozi wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa, Mhe. Ombeni Sefue akimpongeza afisa wake Dkt. Justin Seruhere kwa kupata Shahada ya Uzamivu kutoka Commonwealth Open University, United Kingdom ( UK) katika pongezi zake zake akimnukuu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuhusu kauli Mbiu yake " Elimu Haina Mwisho",Balozi amewaasa wafanyakazi na kila mtu kuwa na kiu ya kujiendeleza bila ya kuchoka na kwamba Dkt. Seruhere ameonyesha njia.
Wanadiplomasia kibao walijitokeza kumpongeza Dkt Justin Seruhere, pichani ni Balozi wa Somalia katika Umoja wa Mataifa, Mhe.Elmi Duale akimpongeza.
Na jirani zetu pia walijumuika nasi, pichani ni Naibu Balozi wa Kenya katika Umoja wa Mataifa Mhe. Josephine Odhiambo, naye akifurahia mafanikio ya Dkt. Jastin Seruhere.
Dkt. Justin Seruhere,Afisa Ubalozi Mwandamizi katika Ubalozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa, akielezea kwa wageni waalikwa hawapo pichani, alivyoianza safari yake ya kuitafuta Shada ya Uzamivu ( PHD) pembeni yake ni Mai Waifu wake Bibi Leonila Seruhere.
Baadhi ya wageni waaalikwa waliofika kumpongeza Dkt. Seruhele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 17, 2011

    Hivi vyuo si ndiyo vipo discredited na research ya Msemakweli Kainarugaba

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 17, 2011

    PhD haina tatizo maana ni mawazo ya mtu binafsi ambapo wengine hawajaweza kuwaza na ufanye machapisho alau matano ambayo yachapishwe. Ndio maana TZ hatuvumbui kitu chenye kuzalishwa kwenye viwanda maana PhD zetu ni mawazo yasiozalishika zaidi ya kuchapishwa tu kwenye majarida ya wanavyuo.

    ReplyDelete
  3. MATANGALUJuly 17, 2011

    Elimu haina mwisho siyo kauli mbiu ya nyerere. Msitake kumpa sifa asiyostahili.

    Kauli mbiu ya nyerere ni "ubepari ni unyama". tehetehehehe.....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...