Naibu Spika Mhe. Job Ndugai (katikati) akiongoza moja wapo ya warsha za wabunge wananchama wa Jumuiya ya Madola CPA kuhusu Misingi ya Mabadiliko katika Bunge (Parliamentary Reforms: Raising the Banchmarks) katika Mkutano wa 57 wa CPA unaoendelea London Uingereza . Mhe Ndugai ni Mwakilishi wa Kanda ya Afrika katika katika CPA Dunia.
Mwakilishi wa Wabunge wanawake Afrika Mashariki katika chama cha wabunge wa Jumuiya ya Madola (CPA) Mhe. Beatrice Shelukindo (Kulia) ambaye pia ni Mbunge katika Bunge la Tanzania akifutilia mada mbalimbali katika warsha ya wabunge wananchama wa Jumuiya ya Madola CPA kuhusu Misingi ya Mabadiliko katika Bunge (Parliamentary Reforms: Raising the Banchmarks) katika Mkutano wa 57 wa CPA unaoendelea London Uingereza. Aliyepembeni ni Spika wa Bunge la Rwanda Mhe. Rose Mukantabana
Naibu Spika Mhe. Jobe Ndugai (katikati) akifanya mahojiano na Mwandishi wa Ben TV Ayoub Mzee mara baada ya kumalizika kwa warsha ya wabunge wananchama wa Jumuiya ya Madola CPA kuhusu Misingi ya Mabadiliko katika Bunge (Parliamentary Reforms: Raising the Banchmarks) ambaye Mhe. Ndugai alikuwa Mwenyekiti katika Mkutano wa 57 wa CPA unaoendelea London Uingereza . Mhe Ndugai ni Mwakilishi wa Kanda ya Afrika katika katika CPA Dunia. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 27, 2011

    Kila leo viongozi mbalimbali wa nchi yetu wanatoka kwenda nje kujifunza/kushiriki jinsi wenzetu wanavyopambana na maisha katika serikali zao.
    Ajabu ya viongozi wetu hakuna hata mmoja ambaye kashafanya mabadiliko yoyote kwenye maendeleo ya nchi yetu.
    Nadhani wapo zaidi kwenye manufaa yao binafsi kuliko taifa lililowapeleka.Sioni umuhimu wa misafara ya aina hii ambayo ni upotezwaji wa fedha za walipa kodi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...