Ankal Salamaleko,


Samahani naomba msaada kupitia blog yetu pendwa ya jamii. Nakupongeza sana kwa kutukabidhi chombo hichi wakati mwenyewe unabaki kumodereti tu. Yaani ghafla bin vuuup mambo ukiyaweka sawa utakuwa facebook ama twitter yetu wamatumbi. Yaani hadi raha na pia huna mfano wala mshindani. Wengine ni fotokopi tu.


Sasa bwana kuna vijimaneno vya kiingereza ambavyo vinanipaga shida sana, hivyo naomba niambiwe maana ama tafsiri zake kama ifuatavyo.


1. Nephew
2.Cousin
3. Niece
Hivi hawa ni kinanani hasa. Yaani kwa kiswahili tuwaiteje? Halafu kuna hili neno 'owe'. Yaani kama nadaiwa natamkaje na kama nadai nasemagaje. Yaani haya yananichanganya kichizi Naomba msaada tafazali.
Ni hayo tu kwa leo, na endelea na kazi nzuri
Wakatabahu
Mdau Mchopa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 26 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 06, 2011

    nephew ni mtoto wa kiume wa dada au kaka,niece ni mtoto wa kike wa dada au kaka,cousin ni mtoto wa mama mdogo/mkubwa au mtoto wa baba mdogo/mkubwa.sina uhakika nafikiri mtoto wa mjomba au shangazi pia wa kike niece wa kiume nephew

    ReplyDelete
  2. nephew -mpwa .mtoto wa dada yako au kaka yako wa kiume
    niece-mpwa.mtoto wa dada yako au kaka yako wa kike
    cousin-binamu
    owe-deni
    hopes thats help

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 06, 2011

    Nephew = Mpwa = mtoto wa dada yako mfano mjombawako atakuita wewe mpwa uwe wa kike au wa kiume haihu

    Cousin = mtoto wa nduguye babako/mamako

    Niece = Kitukuu =mtoto wa mjukuu wako

    Kama unanidai utasema .. "I owe you"

    Kama ninakudai utasema .." You owe me"

    nafikiri itakusaidia kwa sasa, ila kuwa mwangalifu lugha ya kiingereza haiendi kwa kukariri na direct translation

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 06, 2011

    Nephew - Mpwa i.e. mtoto wa dada yako wa kiume ambae atakuita mjomba kama wewe ni mwanaume

    Cousin - Binamu i.e. mtoto wa shangazi yako

    Niece - Mpwa i.e. mtoto wa dada yako wa kike ambae atakuita mjomba kama wewe ni mwanaume

    Pwa wenzetu wametofautisha wakati wakati sie ni neno moja awe wa kike au kiume

    Mdau Igwamanoni wa Itabagumba

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 06, 2011

    Nephew - mtoto wa kiume wa kaka au wa dada
    Niecce- mtoto wa kike wa kaka au wa dada
    cousin- mtoto wa kike au wa kiume wa mjomba au wa shangazi,
    Neno owe,lisikupe taabu,kama unajua matumizi ya NINA BUDI AU SINA BUDI kwamba maneno haya yanatumika kama kinyume nyume vile,basi hata neno OWE,litumie hivyo hivyo kwenye kudai au kudaiwa.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 06, 2011

    http://www.kamusi.org/?q=en/dictionaries

    Asalaam Aleykum
    Miye binafsi napenda sana kusambaza lugha ya kiswahili.
    Swahili is my mother tongue na hata hivyo bado kila siku najifunza.
    Copy and paste the above link onto your browser
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 06, 2011

    Nephew ni mtoto wa kiume wa kaka yako au dada yako au mdogo wako
    Cousin ni binamu
    Niece mtoto wa kike wa kaka yako au dada yako au mdogowako

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 06, 2011

    Mdau
    Nephew=Mpwa(Mwanamke) Mtoto wa dada yako
    Cousin=Binamu(mtoto wa mjomba au shangazi anaweza kuwa mwanaume au mwanamke)
    Niece=Mpwa(Mwanaume) Mtoto wa dada yako

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 06, 2011

    Niece (Mpwa)

    1. a daughter of a person's brother or sister.
    2. a daughter of a person's spouse's brother or sister.

    Nephew (Mpwa)

    1. a son of one's brother or sister.
    2. a son of one's spouse's brother or sister.
    3. an illegitimate son of a clergyman who has vowed celibacy(used as a euphemism).

    Cousin (Binamu)
    1. Also called first cousin, full cousin, cousin-german. the son or daughter of an uncle or aunt.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 06, 2011

    ni hivi mzee
    Nephew-- ni mpwa wako wa kiume (Mtoto wa kiume wa dada/kaka yako)
    Cousin---Ni Binamu wako (yaaani Mtoto wa shangazi/mjomba wako)
    Niece ---ni mpwa wako wa kike (Mtoto wa kike wa dada yako/kaka yako)
    owe--- ni kudai/ kudaiwa
    e.g. I owe you Tsh 20 maana yake Unanidai sh 20
    You owe me Tsh 20 maana yahe NINAkudai sh 20

    ndivyo nijuavyo mm mzee

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 06, 2011

    1. Nephew - = mpwa -mtoto wa kiume
    2.Niece -mpwa lakini wa kike
    3. Cousin - binamu ...................upo hapo?

    Neno: "owe" ni kudai au kudaiwa hasa "pesa" au kitu cha thamani, sasa jinsi linavyotumika:

    Ukisema: I owe him/her - Ananidai
    Ukisema: He/she owes me -ninamdai...........Upo hapo?
    Neno owe unaweza kulitumia kwenye misemo mbali mbali kama ilivyo kwa kiswahili, unaposema mfano: 1."namdai salamu zangu" 2. najua unanidai sijaja kukutembelea n.k....
    Haya bana...najua umepata maana ulizokuwa unazitafuta

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 06, 2011

    1. Nephew = Mpwa (wa kiume)
    2. Niece = Mpwa (wa kike)
    2. Cousin = Binamu

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 06, 2011

    Nephew - Mtoto wa KIUME wa kaka au dada yako au mtu yeyote ambae anakuwa kam akaka au dada yako kwa sisi waswahili vile tuna extended (iliyoongeza family) kwa hiyo mtoto kama wa binamu yako vile ni nephew as well. (LA msingi ni nephew inatumika kwa wa kiume tuu)
    NIECE -ni mtoto wa kike kwa mantiki hayo hayo hapo juu (la msingi NIECE ni wa KIKE tuu)

    Cousin -hapa ni binamu yako na nikiwa na maana ya pande zote mbili so mtoto wa mjomba wako,shangazi yako, baba yako mdogo na mama yako mdogo hawa wote ni couzins wako na kama nilivyosema hapo juu kw asisi waswahii na extended family zetu basi mpaka wale jirani zako ambao umekua nao kama ndugu utawaita couzin mbele ya watu wasiowajua zaidi undani wote yote imetoka hiiiyo.

    owe -mie mwenyewe bado inanipa utata utumiaji wake na ndio ninaishi huku ughaibuni kulikoanzia hiyo lugha soo hapa siwezi kukusaidia samahani sana......
    mdau

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 06, 2011

    Nijuavyo mie niece ni binti wa kaka au dada yako yeye atakuita shangazi , mjomba, baba mdogo au mkubwa, mama mdogo au mkubwa.(Mpwa wa kike)
    Cousin ni binamu kwa maana ya mtoto wa mjomba au shangazi aijalishi jinsi( me or ke)
    na Nephew ni mtoto wa kiume wa kaka au dada yako atakuita mjomba au shangazi,baba mdogo au mkubwa, mama mdogo au mkubwa (mpwa wa kiume)

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 06, 2011

    Tafuta kwenye dictionary kwenye mtanda ya English to Swahili utapata majibu yako hapo

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 06, 2011

    i owe you - unanidai
    you owe me - nakudai

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 06, 2011

    NIMEPENDA WACHANGIAJI WOTE KATIKA MADA HII,WATU WAMEONYESHA UELEWA NA UKOMAVU,KILA MAWAZO YA MTU YAMEHESHIMIWA ,HAKUNA LUGHA YA MATUSI HATA KIDOGO,TUENDELEE HIVI HIVI HII NI BLOG YA JAMII ,ASANTENI SANA.

    ReplyDelete
  18. kazi kweli kweli, job true true.

    = = =
    Buffalo,
    New York

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 06, 2011

    NIECE - (Mpwa) Mtoto wa Kike wa Kaka au Dada yako..
    NEPHEW - (Mpwa) Mtoto wa Kiume wa Kaka au Dada yako..
    COUSIN - (Binamu)Ni mtoto wa Kike au Kiume wa ndugu wa Baba au Mama
    yako...
    OWE - Kama unadaiwa inakuwa I Owe You..
    Kama unadai inakuwa You Owe Me..
    Huo ni mtazamo wangu kwa maelewo yangu lakini mimi siyo mtaalamu wa Lugha

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 06, 2011

    Kaka supu,huyu braza kweli ameishiwa!! na mnaomfahamu msaidieni,atakuwa maralia imemkwea kichwani.Sasa la kujiuliza ni kwamba,umri wote huo haya ni mambo ya kuuliza watu mtandaoni?hapo jirani hakuna shule ya kata? hakuna walimu wa kata?Jamani jamani!!tusiwe washamba kupita kiasi.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 06, 2011

    Wswahili bwana!!! Jamaa anataka kujua WANAITWAJE KWA KISWAHILI we unamuambia "mtoto wa kiume wa dada", mtot wa kike wa kaka"!!! Hayo yote ya nini sasa. Badala ya kutafsiri(translate),mnafasiri(Define). Mnachotakiwa mtoe DEFINITION, sio TRANSLATION. Jamaa anajua kabisa kuwa ni mtoto wa mjomba wa kaka au wa dada, sasa kwa kiswahili wanaitwaje?
    Labda mi nimsaidie kwenye swali analouliza juu ya neno la Kiingereza OWE.
    Nalifafanua neno hili kwa kulitungia sentensi:
    I owe you ten thousand shillings - Unanidai shilingi elfu kumi.
    You owe me ten thousand shillings - Ninakudai shilingi elfu kumi.
    Neno hili huwachanganya watu wengi kwa kutaka kufanya tafsiri ya moja.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 07, 2011

    Nimejaribu kupitia majibu yaliyotolewa kuhusu;
    NICE, NEPHEW, COUSIN, na OWE ni kagundua kuwa wachangiaji wengi wameeleza vizuri maana ya "Owe" kuliko nahau nyingine.Tatizo limejitokeza baada ya tofauti zinazotokana na tamaduni fulani kujitokeza katika tafsiri. Kwa mfano,wakurya humuita mtoto wa mama mdogo 'Binamu'. Wengine humuita kaka au dada kulingana na jinsia. Tofauti hizo zimeathiri tafsiri zinazotafutwa na kumfanya muuliza swali aanze kuwa makini na baadhi ya majibu. Ili kuondokana na ugumu huo, napendekeza kwamba tafsiri itolewe bila maelezo; mfano Binamu- Cousin, Nephew (Mpwa-Kiume), Niece (Mpwa-kike), bila kutoa ufafanuzi ambao ki-msingi unatokana na mila flani au kabila.

    Mzee wa Bondeni kwa Madiba (anayetumia kiswahili ughaibuni).

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 07, 2011

    Wewe uliyedai kuwa muulizaji ameishiwa, mbona unachafua hali ya hewa? Mbona wenzako wamechangia bila ya kumkejeli wala kumtukana muulizaji? Kuuliza siyo ujinga na elimu siyo lazima uipatie tu shuleni. Mimi nimefurahishwa na alivyouliza na namna alivyojibiwa na wadau kwani majibu hayo yatawasaidia hata na watu wengine waliyokuwa hawajui. NA HAYO NI MOJA YA MATUMIZI MAZURI YA MTANDAO.

    ReplyDelete
  24. AnonymousJuly 07, 2011

    huyu mchangiaji wa jul06;07;47;oo pm anatakakuharibu hali ya hewa woote wachangiaje wamemjibu muuliza swali kistaarabu lakini yeye akataka kuleta zake iliaonekane yeye ni mjuaji zaidi si ungekaa kimya kwani lazima uchangie wote hapo juu wamemjibu vizuri wewe mara maleria mara umri wote huu yote ya nini usiukae kimya kwani lazima uchangie umeniudhi sana watu wengine kwakuvunja wenzie moyo hamjambo

    ReplyDelete
  25. AnonymousJuly 07, 2011

    Anon wa Jul 07,01:01:00 AM Wakurya hawajakosea kabisa kumuita mtoto wa Mama mdogo BINAMU kwa ufupi ni sisi waswahili ndiyo tunakosea tunapowaita ndugu za wazazi wetu Mama mdogo au Baba mdogo tulitakiwa tuwaite MJOMBA ndugu zote wa kiume waliozaliwa pamoja na wazazi wetu na Kuwaita SHANGAZI wale wote wa Ndugu wa Kike waliozaliwa pamoja na wazazi.. Kwa ufupi ni matumizi mabaya ya lugha au ufahamu ndiyo maana tunawaita Mama Mdogo au Mama Mkubwa, Baba Mdogo au Baba Mkubwa..

    ReplyDelete
  26. AnonymousJuly 07, 2011

    kwa kukurahisishia nianze na neno "owe",tumia njia rahisi tu kulikumbuka jinsi ya kulitumia,PALE KIDOLE CHAKO KINAPOELEKEZEA MARA YA MWISHO,huyo ndiye mdai, mfano kama kidole chako kitakuelekea wewe ukisema 1. you owe "ME" inamaana wewe ndiye mdai, na kama ni 2. i owe "YOU" Yeye ndiye mdai,3.he owe "HIM","HER" "US" "THEM" n.k zingatia tu kidole chako kinaelekea wapi kwa mara ya mwisho.

    kuhusu nephew-hutumika kwa mtoto wa kiume wa ndugu zako wawe wa kiume ama wa kike.
    niece-hutumika kwa mtoto wa kike wa ndugu zako wa karibu wakike ama wa kiume9kaka zako,dada zako,kaka au dada wa mkeo/mmeo)
    cousine-huyu ni mtoto wa kike ama wa kiume wa ndugu za baba yako au mama yako,hawa ndugu kwa kimombo wale wote wa jinsia ya kiume huitwa uncle,na wa jinsia ya kike huitwa auntie, sio kama sisi waswahili tutavyo baba mdogo/mkubwa,mama mdogo/mkubwa, then ndo shangazi na mjomba la hasha!kimombo ni mjomba/shangazi full stop. ndiyo maana kwa kimombo huwezi kumuita kijana wa kaka wa baba yako BROTHER au SISTER, hawa ni cousine tu.na huyo mzee ni uncle tu kama kawaida.
    nadhani imekuwa clear.
    hivo vyo basi;
    nephew-mpwa wa kiume,
    niece-mpwa wa kike.
    cousine-binamu wakike au wa kiume.
    Dr.phillip

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...