Wafanyakazi wa kiwanda cha kuzalisha soda cha Coca Cola Kwanza, kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, wakiwa katika mgomo wao jana asubuhi. Wafanyakazi hao waligoma wakishinikiza uongozi wa Kiwanda hicho uwaongezee mishahara.
Baadhi ya wafanyakazi wakiongea na waandishi wa habari.
Kiongozi wa TUICO alifika kuwatuliza wafanyakazi hao na kuahidi kuzungumza na Menejimenti ya Kiwanda hicho.Mpaka majira ya saa sita mchana jaan,mgomo ulikuwa unaendelea na Uongozi wa kiwanda hicho ulikataa kuzungumza chochote na waandishi wa habari.Picha zote na Victor Makinda
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...