Kwa uwezo wa Allah na ushirikiano wa hali ya juu uliopo kati yetu (watanzania wa ugiriki) tumeweza kufanikisha mchango wa kumsafirisha mwenzetu SAIDI HASSAN MGOI (Maarufu kwa jina la CHANCE- pichani juu) ili akazikwe nyumbani. Mwili wa Marehemu utawasili Dar J'mosi13/08  saa NANE NA NUSU USIKU kwa ndege ya shirika la Uturuki.
Marehemu alikoshwa,alikafiniwa na kuswaliwa katika msikiti wa ELSALAAM uliopo Neos Kosmos Athens.Idadi kubwa ya watanzania walihudhuria  msikitini.
Taarifa tulizo nazo khs maziko yatafanyika J'pili 14/8 saa saba mchana Tandika Mikoroshini kwa SANDARI ila kwa maelezo kirefu fanyeni mawasiliano na FATUMA dada yake (0718567537) au (0783694736)
 Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi Amin.
INNA LILLAH WAINNA ILAIH RAAJIUUN
Kayu Ligopora
                                KATIBU wa JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI
 WADAU WAKISUBIRI NJE YA MASJID EL SALAAM JIJINI ATHENS, UGIRIKI
 WADAU WAKISUBIRI NJE YA MASJID EL SALAAM- ATHENS
WADAU WAKISUBIRI NJE YA MASJID EL SALAAM- ATHENS

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. mimi nilishakaa hapo umangani enzi hizo tunaishi wengi magheto ya kule Piraeus pale magheto mane.Enzi zile hatukuwa kama mlivyo sasa mnashikamana sana sisi tulikuwa tunangojea meli tuzunguke. Nawaombeeni moka awazidishieni moyo wa huruma maana kwa maisha ya leo watu kuchangishana siyo rahisi na huu ni ukweli usiokatalika.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...