Hello wadau
ajali hii imetokea mchana wa leo  saa saba na robokaribu na sealander brige magari matatu yamegongana chanzo kikiwa ni gari la wagonjwa la manispaa ya kinondoni kufunga breki ghafla likiwa kwenye mwendo wa kasi likielekea Hospitali ya Taifa Muhimbili hivyo kusababisha magari matatu nyuma kumgonga na yenyewe kugongana.
Picha Na Mdau Paul 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. hapa inaonyesha haya magari yaliyogogana ni wale jamaa wanaopenda kuchukua advantage ya ambulance kukwepa foleni kujifanya nao wako kwenye msafara huo. We utawezaje kuifuata ambulace kwa kasi na kwa karibu hivyo? Hiyo ndio faida ya ujanja mwingi!

    ReplyDelete
  2. Poleni kama mmetoka salama.Na hilo 'cruza' lilikuwa na mgonjwa au?Atakuwa ameshtuka sana kama alikuwemo.Pili msongamano wa magari Dar unafanya madereva wengi tunasahau umbali wa kuacha kati yako na mwenzio aliye mbele yako.Kama umbali unatosha hata mwenzako mbele akisimama ghafla unakuwa na muda/umbali wa kutosha kuweza kusimama ghafla(Ref.Defensive driving).Dar ukiacha 'Gap' kati yako na wa mbele yako mwenzio anakuja anachomeka kwenye hiyo nafasi!.Nilifanya utafiti kwenye foleni, gari zinaachana 1/2mita hadi mita 1 tu kwa kuogopa 'kuchomokewa'!Ni hatari

    David V

    ReplyDelete
  3. Nakubaliana kabisa na MDAU WA KWANZA. Hii ni tabia ya madereva wa Dar; wanajifanya wajanja; hawajui maana ya kuheshimu magari ya dharura; na pia umuhimu wa kuacha nafasi kati ya gari na gari. Kama gari iliyo mbele yako ikiharibika na umeacha tu sentimita 30 kati yako na mtu wa mbele; na anayekufuata hivyo hivyo; si mtakesha hapo?Madereva wengine hawana ustaarabu.Ukiacha gap kidogo;unapigiwa honi; au kuchomekewa.Hata mtu akigongwa hivi; ndani ya mwezi anarudia yale yale.HATUJIFUNZI. Cha msingi hakuna aliyeumia; na Cruiser 1HZ hard top bado iko shwaaaaaaari. Mnyama huyo!
    Somo kwa madereva wanaofukuzia gari za Emergency Services; Fire/Ambulance/Police, au hata magari ya kawaida. IT IS ILLEGAL!!!
    Quote: TAILGATING is the practice of driving on a road too close to the vehicle in front, at a distance which does not guarantee that stopping to avoid collision is possible. Approximately one third of rear-end collisions involve TAILGATING.
    In many jurisdictions this action is ILLEGAL and punishable by LAW

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...