Kiongozi wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' Nyoshi El Sadat (wa pili kushoto) akiwaongoza wasanii wenzake katika kulishambulia jukwaa katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.
Msanii wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' Pablo Masai akikonga nyoyo za wakazi wa mji wa Songea katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.
Wanenguaji wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' wakifanya vitu vyao katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wapenzi wa muziki mjini Songea wakiselebuka katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...