MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI  IDDI AKIWA NA MAZUNGUMZO NA  MKURUGENZI WA SHULE YA MBARALI  BW, ALI  PANDU HAJI KATIKA MAZUNGUMZO YAO BALOZI SEIF AMESEMA  MCHANGO UNAOTOLEWA NA SHULE BINAFSI  UNASAIDIA SERIKALI  KWA KIWANGO  KIKUBWA  KATIKA  KUPUNGUZA  MZIGO WA KUWAHUDUMIA  WANAFUNZI  NCHINI 
 
MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI  IDDI  AKIMKABIDHI  MKURUGENZI WA SHULE YA MBARALI BW, ALI  PANDU  HAJI SHILINGI  MILIONI  MOJA  NA NUSU IKIWA NI UTEKELEZAJI WA AHADI ALIYOITOWA  WAKATI  WA  MAADHIMISHO YA MIAKA KUMI TOKEA  KUANZISHWA  KWA  SHULE  HIYO.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema  mchango unaoendelea kutolewa na  skuli   binafsi umewezesha kuisaidia serikali kwa kiwango kikubwa katika kupunguza mzigo   wa kuwahudumia wanafunzi maskulini.

Balozi seif amesema hayo hapo Afisini kwake Vuga wakati akikabidhi shilingi milioni moja na nusu kwa uongozi wa skuli ya Mbarali ikiwa ni utekelezaji wa ahadi   aliyoitowa wakati wa maadhamimisho ya miaka kumi tokea kuanzishwa kwa skuli hiyo.

Fedha hizo ni ahadi ya kwanza  miongoni mwa alizoahidi tarehe 16/7/2011 kusaidia madeski ya darasaa moja, kompyuta moja, milioni moja kusaidia  ununuzi wa madaftari, na shilingi laki tano kwa vikundi vya wanamichezo na wasanii waliotumbuiza siku ya sherehe hiyo.
Balozi Seif amesema  sekta ya elimu nchini hivi sasa ni ya kuridhisha kutokana na mchango huo wa skuli binafsi licha ya changamoto zinazoikabili serikali katika ukamilishaji wa baadhi ya vifaa.
Amesema Skuli nyingi bado hazijawa na madeski na juhudi zinaendelea kuchukuliwa ili kuona tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi kwa kushirikiana na taasisi na mashirika ya maendeleo.
“ Kima cha Madeski kwa Skuli zote za Unguja na Pemba  kimekadiriwa kuwa  Madeski 35.000 kiwango ambacho bado ni changamoto kwa Serikali ”. Alisema Balozi Seif.
Balozi Seif   amefarahisha kwamba Serikali bado inaendelea kukabiliana na kazi kubwa ya kuzijengea uwezo wa  Kimaabara  skuli zake  kwa lengo la kuimarisha Somo la Sayansi.
Amesema hatua hiyo inakusudia kuongeza kiwango cha wanafunzi wa fani hiyo ambayo bado iko chini hasa ikilinganishwa na ukuaji wa sayansi na teknolojia uliopo Duniani hivi sasa.
Amesema mazingira hayo yatawapa fursa Vijana  kufikia lengo la kuwa wataalamu mahiri wa Taifa   hapo baadaye.
Akipokea msaada huo Mkurugenzi wa Skuli ya Mbarali Bwana  Ali Pandu Haji amempongeza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwa Juhudi zake za kusaidia Skuli Binafsi.
Bwana Pandu amesema katika kuunga Mkono juhudi za Serikali Uongozi wa Skuli ya Mbarali umeweka Kiwango kidogo cha ada ya wanafunzi ili kumuwezesha kila mtoto anapata Haki yake ya Elimu na msingi.             .. 

Imeandaliwa na Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 
2/9/2011.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...