Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amewaapisha wakuu wa mikoa aliowateua hivi karibuni.Sherehe za kuwaapisha wakuu hao wapya wa mikoa imefanyika leo asubuhi katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam.Pichani ni Mkuu mpya wa Mkoa wa Tabora. Bi.Fatuma Mwassa akila kiapo mbele ya Rais Dkt. Jakaya Kikwete na kukabidhiwa miongozo ya kazi.(picha na Freddy Maro).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Huyu Fatuma Mwasa tunamfahamu sana tu,alikuwa muandishi wa habari wa mitaani tu,akapachikwa ukuu wa wilaya Mvomero sasa mkuu wa mkoa,Hii inadhihirisha kuwa katika serikali yetu watu hupewa vyeo kwa kujuana,na hicho kitu kinasababisha nchi hii kuwa na matatizo sugu,watu wanaaaowekwa madarakani na rais wengine hawana qualiicatins zozote wala experiance ya uongozi,bali wanajuana na rais au ni marafiki wa first lady.Inasikitisha sana haijulikani tutakakoishia ni wapi na hii system.Uonevu na ufisadi utakwisha tu Tanzania na siku itafika,maana hata Gadaffi haamini yanayoendelea nchini mwake.amebaki kujificha kama panya.Mungu ibariki Tanzania yetu ya mateso na ufisadi.

    ReplyDelete
  2. Keep it up dada Fatuma Mwassa, hongera sana

    ReplyDelete
  3. Pole yako kama huna wa kukuweka kwenye nafasi ya juu.
    Sidhani kama unamfahamu dada Fatuma vilivyo, alikopitia baada ya uhandishi wa habari?!
    Na sidhani kama unajua kazi alizozifanya Mvomero, utabakia kua HATER tuu.. Pole sana anon wa kwanza..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...