Kituo cha utafutaji na uokoaji majini (MRCC) kinachoratibiwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), kimepokea taarifa za kushambuliwa kwa meli ya utafiti wa mafuta iitwayo Ocean Rig Poseidon. 


 Tukio hilo limetokea tarehe 3/10/211 saa 2:15 usiku, umbali wa maili za baharini 23 kusini mashariki ya kisiwa cha Mafia sawa na maili 82 kutoka Dar es salaam.

Katika tukio hilo maharamia 7 waliokuwa katika boti ndogo waliishambulia meli hiyo kwa silaha. Mashambulizi hayo yalijibiwa na walinzi wa meli na Jeshi la Wanamaji wa Tanzania na maharamia walidhibitiwana kukamatwa na wanashikiliwa mikononi mwa jeshi la Wanamaji.

Imetolewa na:
E.S Wapalila
K.n.y: Msajili wa Meli

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. kazi nzuri sana waliofanya ulinzi hapo hii habari itapeleka ujumbe hatutaki maharamia huku

    ReplyDelete
  2. Duuuh hawa jamaa sasa wamezidi! Nafikiri sio wasomali peke yao lazima kuna mikono ya watu wengine.

    ReplyDelete
  3. hao ni kuwadhibiti tu haiwezekani wakatuchezea namna hii lazima wachukuliwe hatua madhubuti

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...