Moja ya watumishi wa kampuni ya AAICO ambayo ndiyo wamepewa dhamana ya kukusanya ushuru wa maegesho ya magari jijini mbeya akitoa mnyororo kulifunga gari la wachina hao huku mama wa kichina akilia kwa hasira
Mama wa kichina akimtolea maneno makali binti Eliza mkusanya ushuru wa maegesho ya magari huku mchina huyo akiendelea kugoma kuwa hawezi lipa ushuru siku ya jumamosi na jumapili kwani ni siku za mapumziko siyo siku za kukusanya ushuru
Mume wa mama  wa kichina akijaribu nae kuwaelewesha wakusanyaji ushuru wa maegesho ya magari kuwa wameshazoea hivyo kutolipa siku ya jumamosi na jumapili kwani ni siku za mapumziko
Mama wa Kichina akiwa amechachamaa na kuelekea katika Jengo la NMB Tawi la Mbalizi Road Mjini Mbeya kuomba msaada kwa Askari Polisi waliokuwepo hapo.Picha na Mbeya Yetu Blog

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Huyo mama wa Kichina asilete za kuleta. Huku kwao wala hakuna kubishana na wala hakuna cha jumamosi au jumapili. Inatakiwa zitungwe sheria ndogondogo kali na majiji au manispaa ili wapuuzi kama hao walipe mara mbili na kwenda jela siku nne ili uwepo utii wa sheria. Kama sheria hizo zipo tunaomba zitumike bila kuangalia rangi.

    ReplyDelete
  2. In all fairness in a lot of places in other countries parking is free on the weekends

    ReplyDelete
  3. Mama wa Kichina yuko sahihi.....Nchii hii ni yetu ila kodi ni nyingi sana

    ReplyDelete
  4. Namuunga mkono...hivi lakini kweli hii sera ya ushuru siku za weekend na mapumziko ni sahihi??? mbona naona kama hawa wachina wana point?? maoni yangu jamani naomba ya kwenu maana natarajia kununua ka bajaji ka kwendea ibada na miss my family...

    ReplyDelete
  5. Nadhani wachina hawa wana haki. Kama Jumamosi si siku ya kukusanya kodi, iwaje watu hawa wakusanye kodi?

    ReplyDelete
  6. Nakubaliana na Wachina 100%. Ningewaona wana dosari endapo tungekuwa tukishuhudia mabadiliko katika miundombinu yatokanayo na huo ushuru, lakini kwa staili hii wakusanye ushuru siku moja tu ya wiki kama kigezo cha ajira.

    ReplyDelete
  7. Nadhani kodi siku ya weekend si sahihi. Nchi karibu zote duniani hazitozi kodi siku ya Jumamosi. Halafu hao jamaa naamini kabisa kuwa hiyo pesa ilikuwa inakwenda mifukoni mwao. Hii Tz bwana, ulaji nje nje kila mtu anajua hata waziri anayeshughulikia masuala ya ushuru, hili analijua. Kama anabisha, muulize kodi ngapi ilitozwa leo jumamosi Mbeya? Hakika hana jubu kwa sababu hajatengeneza mfumo wa kudhibiti mapato ya kodi. Watoza kodi wasiibe hapo. Mtuuumeee!

    ReplyDelete
  8. Inategemea. Kuna sehemu jumamosi wanatoza parking fee na kuna sehemu hawatozi. Uamuzi ni watu wa Mbeya wameweka utaratibu upi. Mdau aliyeko China, hawa wa China bom sana mimi ninao hapa Ukerewe wanajipendekesa sana kwa wakerewe tena wanachukua maneno kwako wanawapelekea wakerewe. Ni watu wanafiki sana tena ningeomba serikali yetu isiwape kila sehemu maana wana agenda za kama wazungu. Angalieni jamani. Wamekuja kujitajirisha kwetu wakajenge kwao!!

    ReplyDelete
  9. Huyo mchina sileta mbwe mbwe hapa. Sheria ni msumeno. Hula mbele na nyuma. Kama utaratibu ni kulipa kodi hadi siku za weekends basi na alipe. Masuala ya kubishana nadhani hayatakiwi. Ni masuala ya kisheria zaidi. Kama weekend haitakiwi kulipa kodi basi itabidi sheria zibadilishwe kwanza. Kwa sasa itabidi alipe tu hata kama akipandiah hasira namna gani. Kwanza huku kwao ni wabaguzi acha.

    ReplyDelete
  10. Wewe mdau wa kwanza kutoa maoni yako, mimi nakushangaa sana.Kwanza si sahihi kutoza ushuru wa maegesho siku zisizo za kazi, halafu pia,hichi hakipo kwenye mada, kwa nini watoleshe watu kodi ya maegesho wakati wao hawajatengeneza hizo parking? wamekuta tayari barabara zimeshajengwa wao wameingilia tu kukusanya hiyo kodi.Wajenge parking kubwa tuone kama watu watakataa kutoa kodi, wao hawaja-invest chochote wanataka kuchukua hela za wananchi bila ya wao kutoka jasho lolote (to invest).Wewe mdau ni MBAGUZI, na wa TZ wengi ni waoga na hawajui hata haki zao na ndiyo maana wamezoea kuonewa, sasa wanapopata watu kama hao wanaojua haki zao ndiyo mapambano yanatokea.Wewe mdau wa kwanza unaishi nchi gani hiyo ambayo hata siku za mapumziko mnalipa kodi za maegesho ya magari.Acha kutudanganya wewe.

    ReplyDelete
  11. Tatizo hizo parking hazinz hata sign za kuonyesha ni muda gani na siku gani mtu anatakiwa kulipia kama kungekuwa na saini hakuna mabishano

    ReplyDelete
  12. HIZO PESA ILIKUWA ZIKUSANYWE KWA AJILI WA BOSS KWANI HATA DAR ES SALAAM HAKUNA KULIPIA PARKING WEEK END, NI KAMA TRAFIC WETU HAPA WANAPANGIWA KITUO CHA KUKUSANYA ETI KWA AJILI YA BOSS MIMI IMENITOKEA NILIPOBISHANA NAE AKANAMBIA NATAKA NIMFUKUZISHE KAZI KWANI PESA YA BOSS HAIJAKAMILIKA NA TATIZO HILO JK ANALIANGALIA TU

    ReplyDelete
  13. Sasa inamaana hizo Parking hazina vibao vinavyoeleza siku na masaa ya Free? kama ni hivyo mgeni atajuaje? wekeni vibao ili kuepuka migogoro kama hiyo.Mbeba box.

    ReplyDelete
  14. WEKA MUDA WA KUPAKI NA SIKU ALAFU MTU ALETE UBISHI, HUYO NILETEE HAPA

    ReplyDelete
  15. nataka kuwaambia ukweli jumapili sio siku ya kazi, na wanadumia document bandia kuibia watu, hao kama unabisha chukua document kaulize ofisini watasema hawaitambui.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...