Huyu ndiye Msamaria mwema aliyemgundua Cecilia Edward huko Kisarawe mkoa wa Pwani na kuamua kumsaidia yatima huyu anayeteseka na maradhi ya moyo na kuvimba tumbo. Juhudu zimefanyika kumpeleka India ambako amerudi bila kutibiwa uvimbe wake wa tumbo. Mikakati zaidi inahitajika ili kumsaidia yatima huyu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. kwa nini wameshindwa kumtibu ?
    mdau paris

    ReplyDelete
  2. Wanandugu!!!

    Kuna Nabii anaitwa TB Joshua yupo pale Lagos Nigeria, ingekuwa vema pia akipelekwa pale kwa maombi yanasaidia sana hasa pale uwezo wa binadamu unapofikia kikomo.

    ReplyDelete
  3. Ni kweli..lisilowezekana kwa binadamu kwa Mungu linawezekana....

    ReplyDelete
  4. Anony Thu Oct 13, 08:10:00 AM 2011...acha mambo yasiokua na msingi. Uyo mtoto anaumwa na magonjwa yanajulikana sasa wewe kutoa ushauri apelekwe kwa matapeli Nigerians sioni kama ni jambo la msingi. Kwa taarifa yako hakuna nabii ulimwengu wa leo na wala hatotokea mpaka Yesu/Jesus/Issa arudi.

    ReplyDelete
  5. Wameshauri atumie dawa kwanza ili kuondoa sumu iliyosababisha maradhi. Sumu iliyotokana kwa kula mihogo. Cha kufanya asaidiwe lishe na kuendelea na dawa.

    ReplyDelete
  6. Hii habari haijakamilikia mkuu. Amerudi bila kutibiwa? Kwa nini? Alienda lini?

    ReplyDelete
  7. Amerudi bila kutibiwa kwanini? Na nini kinacho takiwa kufanyika hivi sasa. Tuko tayari kusaidia...

    ReplyDelete
  8. Nashauri aliyemtoa Mgonjwa kisarawe,asaidiwe kusafiri kwenda TB Joshua,Lagos Nigeria kama alivyoshauri mtu mmoja hapo juu.NAAMINI MTOTO ATAPONA TENA ATASHANGAZA WATANZANIA.

    ReplyDelete
  9. Tafadhali naomba namba ya simu ya anayemtunza huyo mtoto,yaani huyo aliyemtoa kisarawe,tushauriane ili tuone cha kufanya.My email is:pdkihoza@gmail.com
    From Joensuu,Finland.

    ReplyDelete
  10. wadau, kwenye kuomba msaada ili akatibiwe maelezo yalikuwa mazuri sana. Nafikiri ingekuwa vizuri vilevile tukaelezwa ni adha gani imetokea ndugu yetu hakufanikiwa kupata matibabu kusudio. Na ikiwezekana tuelezwe hata kitaalamu ijapokuwa sisi wataalamu wabongo tulilishindwa sakata lake. Hi itatujengea sisi wataalamu nakishi ya kugundua wengine mapema kabla hali haijawa kama ya huyu aliyerudishwa. Sumu ya Mhogo? possible!!, but are you serious, and which one might be, how it affect human body,and what will be the management plan (treatment). Yah, anything is possible in medicine BUT we need explanation as why she is back without any intervation.

    ReplyDelete
  11. Inasikitisha kweli, sasa India kwanini wanamrudisha hivi hivi? Hiyo sumu imeshindikana kweli hospitali? unawarudishia familia ambao hawana uwezo in the first place kwamba waondoe sumu?? How

    ReplyDelete
  12. Inasikitisha kweli, sasa India kwanini wanamrudisha hivi hivi? Hiyo sumu imeshindikana kweli hospitali? unawarudishia familia ambao hawana uwezo in the first place kwamba waondoe sumu?? How

    Sijui ni gharama au vipi ila serikali ingesaidia kiasi ili aendelee kukaa ili watafute dawa za kuondoa sumu pole pole. Otherwise hii ni kupunguza siku za maisha ya mtoto mzuri kama huyu...inasikitisha sana

    ReplyDelete
  13. Asante sana msamaria mwema kwa kazi yako. tuwasiliane tuone tutasaidia vipi.Nitashukuru kama utaweza kunieleza kiurefu na ukweli kuhusu ni nini kinahitajika ili cecilia apone. Na matokeo ya matibabu india. asante
    kokodemelo@yahoo.com
    pat

    ReplyDelete
  14. Jamani ila madaktari wamesema atumie dawa kwanza nyie semeni tu mara mganga,nabii, shehe na maombi ila mkumbuke kila kitu na Imani ya mtu, hamwezi kumchukua mkristo kumpeleka kwa shehe wala muislamu mumpeleke kwa nabii. Hivyo naomba msipandikize kitu ambacho hakipo kwa mtoto.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...