Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(watatu kushoto),Balozi  Juma Mwapachu(kushoto), Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal(wapili kushoto), Rais Mstaafu awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi,(wanne kushoto) na Waziri Mstaafu Bakari Mwapachu(kulia)wakiwa katika swala ya kumuombea Marehemu Harith Juma Mwapachu wakati wa mazishi yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo mchana.Marehemu Harith aliyefariki jana asubuhi ni Mtoto wa kiume wa balozi Juma mwapachu
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la marehemu Harith Juma Mwapachu aliyefariki jana asubuhi na kuzikwa leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo mchana.Kulia nia Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal ambaye pia alishiriki mazishi hayo.Marehemu Harith ni mtoto wa kiume wa Balozi Juma Mwapachu katibu mkuu mstaafu wa jumuiya ya Afrika Mashariki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Afali Kikwete wamemuwekea viti viwili maana hivi viti vya plastic vinaangusha watu sana,visije muangusha rais

    ReplyDelete
  2. Mwenyez Mungu ampe moyo wa subira Balozi Mwapachu kwa msiba huu wa ghafla wa kupoteza mtoto/kijana..inaumiza sana..kwa sisi ambao yametukuta tunaelewa but Mungu ni mwaminifu kwetu siku zote..May his soul rest in eternal peace..Amen

    ReplyDelete
  3. POLENI WAFIWA

    ReplyDelete
  4. hata kofia jamani? poleni hata hivo?

    ReplyDelete
  5. inaa lilahi waina illahim rajiun poleni sana family ya mwapachu kwa kuondokewa na mpenzi wao. nilisoma naye marehemu. poleni sana inna lillahi waina illahi rajiun.
    new york marekenai.

    ReplyDelete
  6. mze ruksa raisi wetu mpendwa ally hassan mwingi nakukumbuka ndugu yangu sana tena sana kwa jinsi ulivyo okoa taifa letu kwenye uchumi mbaya mungu akubarik na hata siku ukienda mbele ya mola wako atakuwa radhi na wewe amin.

    salaam toka london

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...