Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Charles Boniface Mkwasa ameteua wachezaji 28 kuunda kikosi hicho kwa ajili ya michuano ya Kombe la Chalenji inatakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Novemba 25 mwaka huu.
Wachezaji walioteuliwa ni Juma Kaseja (Simba), Deo Munishi (Mtibwa Sugar) na Shabani Kado (Yanga). Mabeki wa pembeni ni Shomari Kapombe (Simba), Godfrey Taita (Yanga), Juma Jabu (Simba) na Paul Ngelema (Ruvu Shooting).
Mabeki wa kati ni Juma Nyoso (Simba), Said Murad (Azam), Erasto Nyoni (Azam) na Salum Telela (Moro United). Viungo ni Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Ibrahim Mwaipopo (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba), Haruna Moshi (Simba), Ramadhan Chombo (Azam), Rashid Yusuf (Coastal Union), Jimmy Shogi (JKT Ruvu Stars) na Mohamed Soud (Toto Africans).
Washambuliaji ni Mrisho Ngasa (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Gaudence Mwaikimba (Moro United), John Bocco (Azam), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Daniel Reuben (Coastal Union) na Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada).
kiko wapi msemo ETI nitaita vijana watupu.Mmeshaanza mashinikizo
ReplyDeleteAngalau umri kidogo umezingatiwa. Nashauri mashindano ya makundi kuwania kombe la dunia yakianza ichukuliwe timu ya vijana kuwakilisha taifa, ili ipate uzoefu na kujengwa kuchukua nafasi badala ya hii tuliyonayo.
ReplyDeleteHaa haaa wewe namba moja umenivunja mbavu kweli..
ReplyDeleteDavid V
Safi sana! About time Ibrahim Mwaipopo kuitwa timu ya Bara(na hopefully Taifa Stars soon!) One of the best defensive midfielders in TZ at the moment. Nimefurahi sana akina Machupa na Shindika kuachwa - wanatupotezea muda tuu wale!
ReplyDelete