Mkurugenzi Mkuu wa Ifakara Health Institute,Salim Abdallah akizungumza na waandishi wa habari juu ya kongamano la kimataifa linalojadili mambo mbalimbali ikiwemo kuboresha hatua za kuwafikishia wananchi dawa za kutibu malaria na udhibiti wa ugonjwa huo kwa kutumia dawa za ALU. Kongamano hilo lilianza leo jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa mipango ya Utafiti ya Ifakara Health Institute Dkt. Honarati Masanja (kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu tafiti mbalimbali zilizofanyika zinazolenga kudhibiti ugonjwa wa malaria katika kongamano la kimataifa linalojadili jinsi ya kudhibiti malaria. Kongamano hilo lilianza leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mhadhiri kutoka Shule inayoshughulikia masula ya Afya ya Jamii katika Chuo Kikuu ) cha Ghana (School of Public Health – University of Ghana) Profesa Fred Binka.
Mhadhiri kutoka Shule inayoshughulikia masula ya Afya ya Jamii katika Chuo Kikuu ) cha Ghana (School of Public Health – University of Ghana) Profesa Fred Binka akitoa ufafanuzi kuhusu tafiti mbalimbali zilizofanyika zinazolenga kudhibiti ugonjwa wa malaria katika kongamano la kimataifa linalojadili jinsi ya kudhibiti malaria. Kongamano hilo lilianza leo jijini Dar es salaam. Kulia Mkurugenzi wa mipango ya Utafiti ya Ifakara Health Institute Dkt. Honarati Masanja.Picha na Tiganya Vincent, Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Watu na majina havipo sawa!!! fanyeni quality assurance kabla ya kurusha

    ReplyDelete
  2. Masahihisho; picha ya kwanza anayeongea ni Fred Binka, picha ya tatu ndio Salim Abdulla

    ReplyDelete
  3. ankali umechanganya maelezo ya picha ya kwanza umeweka picha ya tatu na maelezo ya picha ya tatu umeweka ya kwanza

    ReplyDelete
  4. 4 50yrs still fighting malaria teh teh teh

    ReplyDelete
  5. Aliyeposti habari hii amechanganya maelezo. Mkurugenzi wa IHI ni huyu ambaye anaonekana kwenye picha ya tatu amesimama na sio yule kwenye picha ya kwanza kama ilivyoelezwa.

    ReplyDelete
  6. Geuza maelezo hayo....mkurugenzi ni salim huyo aliesimama picha ya chini hapo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...