Na Anna Massao (IUCO)

Mkutano wa kimataifa kujadili masuala mbalimbali ya ardhi wenye jumla ya nchi wanachama kumi na nane kutoka Afrika unaendelea jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Double tree. Mkutano huo ulifunguliwa jana na katibu mkuu wa wizara ya ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi Patrick Rutabanzibwa ambao ni mkutano wa maandalizi wa makatibu wakuu utakaoanza 17 Novemba.

Lengo kubwa la mkutano huu ni kusaidia nchi za Afrika katika masuala ya upimaji na ramani kwa ajili ya maendeleo ambapo mkutano huu ni wa 45 kufanyika baada ya ule wa Capetown, South Afrika na Tanzania ndio mwazilishi wa kituo hiki mwaka 1975 chenye makao yake makuu jijini Nairobi na unajumuisha nchi kumi na nane zikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan, Ethiopia, Botswana ,Namibia , Zambia, Mauritius, Seychelles , Somalia, Comoros , South Africa, Rwanda, Burundi , Lesotho ,Malawi and Swaziland.

Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni mkurugenzi wa upimaji na ramani katika wizara ya ardhi Mr Silas Mayunga anasema, ‘tunafarijika kupata fursa ya kuaandaa mkutano huu, maazimio yatasaidia katika kuimarisha shughuli za upimaji ardhi, utunzaji wa mazingira na mafunzo kwa wataalamu na pia nchi yetu imejitangaza,’

Mr Mayunga aliongeza kuwa Tanzania ni nchi ya kwanza barani Afrika kukamilisha mpango wa alama ya upimaji ardhi inayojulikana kitaalamu ‘geodetic network’ambazo ni 740 na kuweza kusimikwa nchi nzima na kuongeza kuwa 6 kati ya alama hizo zimepimwa kitaalamu kwa njia ya satelaiti na pia serikali ina mpango wa miaka mitano wa upimaji ardhi nchini na katika kutekeleza mpango huo serikali imekubali kuanzisha kituo cha kupokea picha za satelaiti kitakachojengwa mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...