Jana Mwalimu Mwanaisha Kikwete alikula Nondozz ya BA. Education kutoka Chuio Kikuu Huria -OUT mahafali yaliyofanyika Kibaha na baadae kukafanyika Maulid Nabii iliyofuatia na dhifa ya chakula nyumbani kwao Mwalimu Kikwete huko Temeke ambayo pia ilihudhuriwa na wifi yake Mama  Salma Kikwete.

  Mwalimu Mwanaisha akiwa na kaka zake Mdau Charles Semiono kushoto na Mdau Abdul Issa Kihenya kulia. 
 Ndugu, jamaa na marafiki wakimpongeza Mwalimu
 Watoto wa madrasa wakighani qasda wakati wa sherehe hiyo
Wifi yake Mama Salma Kikwete akitoa pongeza na nasaha kuwahimiza kinamama nchini kufuata mfano wa Mwalimu Mwanaisha kuwa Elimu haina mwisho na kwamba Wanawake wakiamua wanaweza!
Picha na Mdau Ankal  Midladjy Maez

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Hongera Mwalimu, lakini ankal ningependa kujua huyu nia Mwanaisha Kikwete au Zainab Kikwete mbona siku ya graduation kule kibaha waliita Zainab Kikwete na sio Mwanaisah.

    ReplyDelete
  2. Hongera sana tena sana dada Mwanaisha, hukujali umri wako ukaamua kujiendeleza mpaka kufikia hapo ulipo, heshima ya mwanamke ni elimu.

    ReplyDelete
  3. SAFI SANA SHEREHE ZA NAMNA HII. SIO KILA SIKU MZIKI TU MAPOMBE,

    ReplyDelete
  4. Hongera Mwl. Mwanaisha Kikwete kwa kujua umuhimu wa Elimu na kuweka msisitizo hadi kupata Shahada!!!.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...