Maandalizi kwa ajili ya Bonanza la tatu la mazoezi ya viungo yameanza rasmi ambapo kilele cha Bonanza hilo  kitafanyika  tarehe 1 ya Januari  2012.
Bonanza hilo linalofanyika kila mwaka ifikapo  Januari 1, 2012 huandaliwa na Chama cha mchezo wa mazoezi ya Viungo Zanzibar( ZABESA).

Katika maandalizi hayo, leo yaliandaliwa mazozi ya pamoja kwa vilabu vyote vitakavyoshiriki katika Bonanza hilo, ambapo vilabu husika vilipangwa kufanya mazoezi kwa kanda kulingana na maeoneo vilabu vinamofanyia mazoezi.

Bonanza hilo litavishirikisha vilabu zaidi ya 24 vya mazoezi ya viungo  Mjini na Vijijini ambavyo kwa kawaida huwa vinafanya mazoezi katika maeneo mbali ya Zanzibar.

Kabla ya Bonanza kunakuwa na wiki ya bonanza ambayo mara hii  itaanza tarehe 24/12/2011  ambapo kutakuwa na michezo  mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba, michezo ya asili kama vile nage, kufukuza kuku nk. Michezo hiyo itakayowahusisha wanachama wa vikundi vya mazoezi katika maeneo mbali mbali ya  Zanzibar.

Katika wiki ya Bonanza, kwa kushirikiana na Benki ya Damu na Zanzibar Outrech Programme (ZOP) kutakuwa na huduma za kuchangia damu pamoja na kupima afya za wanamazoezi, hasa kupima sukari, presha, macho, koo na masikio na wananchi bila ya malipo.

Lengo kuu la bonanza hili ni kuwahamasisha wananchi kufanya mazoezi ya viungo kwa ajili ya kujenga afya zao. Aidha bonanza hili linatoa fursa ya kuvikutanisha vilabu vyote vya Zanzibar vinavyofanya mazoezi ili kuonana, kubalishana mawazo, kuelimishana na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa mazoezi ya viungo kwa ajili ya kuimairisha afya zao kwa ujumla pamoja na kujenga uhusiano mwema na Serikali na taasisi nyengine za kijamii.

Mgeni rasmi katika Bonanza hilo atakuwa ni  Makamo wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad  ambae atayapokea rasmi maandamano ya vilabu hivyo katika uwanja wa Amani na kuwahutubia wana mazoezi na wananchi kwa jumla.

Washiriki Bonanza hilo watakuwa ni wana  vilabu mbali mbali vya mazoezi wakiwemo wanawake, wanaume, vijana na watoto, Makocha wa vilabu na viongozi wao, Wabunge, wawalikishi, Mawaziri wa SMZ; Maafisa mbali mbali wa serikali, viongozi  wa mikoa  na wilaya, Waandishi wa habari, Wasomi na Wananchi kwa ujumla. Pia bendi ya Magereza itaongoza matembezi  ili kunogesha shehehe hizi.

Maandamano ya wanamazoezi yataanza saa 12 kamili asubuhi siku ya Jumamosi ya tarehe 01 Januari 2012, katika bustani ya Michenzani-Muembekisonge kuelekea uwanja wa Amani, kupitia Kijangwani, Mfereji wa wima, Mikunguni na kuishia Uwanja wa Amaan na kutakuwa na matembezi ya mchaka mchaka.
Wito unatolewa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika kushiriki Bonanza ikiwa ni katika kujiunga na matembezi, kushuhudia au kutuo michango mbali mbali itakayofanikisha shughuli hiyo.
FANYA MAZOWEZI, IMARISHA AFYA YAKO





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera kwa kuwa ufahamu wa umuhimu wa mazoezi kwa afya. Pia msisahau kuangalia ulaji wenu. Msisahau kupia Mchamba Wima!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...