TAARIFA ya iliyotufikia hivi punde katika inaeleza kuwa mbunge wa jimbo la ARUMERU kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Mh. Jeremia Sumari (pichani) amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili mara baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mh. Jeremia Sumari ni mbunge wa pili kufariki dunia kwa mwaka huu 2012 kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kutanguliwa na Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Morogoro,Marehemu Regia Mtema aliyezikwa nyumbani kwao Ifakara Mkoani Morogoro jana na mazishi yake yaliongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Kikwete.

Globu ya Jamii inaendelea kufuatilia taratibu zote za msiba huu na tutaendelea kutoa taarifa kadri zitakavyokuwa zikitufikia.

Mungu ailaze roho za marehemu mahala pema peponi

-Amen

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. haya Tendwa lalamika sasa kuwa ni bilioni 19 nyingine hizo za uchaguzi!

    ReplyDelete
  2. Poleni familia ya marehemu,ndugu jamaa na marafiki na vyama vyote vya siasa,mungu awape muongozo ktk msiba huu.

    ReplyDelete
  3. Duh,poleni familia, poleni serikali,BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIBARIKIWE

    ReplyDelete
  4. this is another tragedy. Poleni sana familia ya mzee sumari. Haya yote ni mambo ya mungu, wote safari yetu ni mmoja.

    NB MSILETE SIASA KWENYE MAMBO YA VIFO.ISSUE YA TENDWA HAPA IS IRRELEVANT. THOUGH YOU HAVE RIGHT TO TALK. ALICHOKIZUNGUMZA TENDA NI KWAMBA KAMA TUNAWEZA KUEPUKA KUTIMUANA INA BORA ZAID. SASA MAMBO VIFO TUTAYAEPUKA VIPI. HACHENI HIZO BWANA.

    ReplyDelete
  5. poleni sana wafiwa

    tendwa alijihusisha kwa kulalamika kuwa cuf inasababisha ghalama nyingine za uchaguzi

    hakuweza kufahamu kuwa jambo lolote linaweza kutokea iwe kisheria au kwa mkono wa mungu

    sasa kuna majimbo mangapi yanahitaji uchaguzi?
    ni ghalama ngapi zitatumika kufanikisha zoezi hilo?

    viongozi wetu sio mnakurupuka tu kwa kutoa hoja binafsi zisizo na point yeyote sasa hapo utamlalamikia nani?

    mungu ibariki tanzania wabariki na watu wake

    mungu waongoze viongozi wetu wa tanzania njia bora na imara yenye mafanikio kwa taifa na wasiwe wabinafsi.

    ReplyDelete
  6. Eee Mwenyezi Mungu ILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI. AMINA.

    ReplyDelete
  7. Mdau wa kwanza sielewi kwa nini umeunganisha sababu za kifo na za kufukuzana. Wewe mwenyewe unajuwa kifo ni swala ambalo binadamu hana udhibiti nalo na tendwa kusema vile alikuwa na maana kuwa vyama vinatumia vibaya nafasi waliyopewa ya kudhamini wabunge ndo maana akawalamikia kuwa ni gharama kwa serikali kwa kuwa kufukuza wabunge hovyohovyo kunasababisha kuwa na chaguzi ndogo ambayo ni gharama kwa serikali. Lakini kamwe hakuhusisha na vifo vya wabunge. Poleni wanfamilia na watanzania kwa ujumla mwenyezi mungu haulizwi mbele kwake nyuma kwetu

    ReplyDelete
  8. Pole Mama Sumari poleni watoto kisali, sioi, Joan na wengine kwa msiba huu mkubwa WA Baba yenu Mpenzi Bwana ametoa na bwana ametwaa jinalake na lihimidiwe.(Ndugu yenu wa LJS) POLENI SANA.

    ReplyDelete
  9. We anon wa Thu Jan 12,12:16:00 pm 2012 Funga domo lako wewe mwenyewe unaendeleza siasa hapa ivi ungekaa kimya ingekuwaje ungekuwa na akili na busara usingetoa hoja hiyo ambapo tayari ulisha ona kuwa ni tatizo.

    ReplyDelete
  10. May He Rest In Peace.

    ReplyDelete
  11. cjui baba rizi na huu ataenda??maan huwa nafikiria sie 2naofanya kaz kwa wahindi 2ngekuwa 2naaga na kuhudhuria misiba ka baba riz cjui ka 2ngekuwa na kazi hadi leo??maana baba rizi anaanzia dar hadi tanga analalia....mungu aiweke roho yake pema pepon

    ReplyDelete
  12. Its so sad! Mungu ampumzishe kwa amani,Amen.

    ReplyDelete
  13. Duh hizi nywele nilifikiri MWAPACHU niliposoma ndio nikakuta SUMARI, poleni wafiwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...