Mojawapo ya picha za mwisho mwisho za  Mwimbaji/mwigizaji Whitney Houston ikionesha akitoka kujirusha na marafiki zake katika kiota cha Tru Hollywood  jijini Los Angeles Alhamisi usiku
 Mwili wa Whitney Houston ukiondolewa katika hoteli ambako inasemekana alikufa akiwa bafuni
Waombolezaji wakiwa wameweka maua na ujumbe wa kumkumbuka Whitney. Chanzo na habari kamili BOFYA HAPA

Kunradhi: Mapema usiku huu ripota wa zamu wa Globu ya Jamii aliweka kimakosa picha na habari kwamba Whitney Houston yu hai bado. Ukweli ni kwamba msanii huyu hatunaye tena na mashabiki wake dunia nzima wanaomboleza. Baada ya kuiondoa haraka habari hiyo, tunawataka radhi wadau kwa usumbufu kutokana na habari hiyo ambayo ilitokea mwaka 2001 na kurushwa hapa  leo kwa bahati mbaya -Michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Mwenezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Tutaendelea kumkumbuka kupitia nyimbo zake tamu. Ametanguli nasi nyuma yake. TAUS KINGI

    ReplyDelete
  2. Sawa na kifo cha mvuta bangi mtaani tu; wote walipaswa kujua madhara ya madawa ya kulevya! Ama kwa kuwa huyu maarufu?

    ReplyDelete
  3. EEh jamani. Hata waliokufa mnawanyanyasa. Watanzania too much.

    ReplyDelete
  4. Tulimpenda na kumkubali sana kwa kupitia music, na sio mihadarati.......kwani ilikuwa ni kitu personal tukinachompa stimu. Mchango wake ktk jamii ulikuwa ni kuimba nyimbo zenye ujumbe maridhawa. Kwa hiyo mnaomponda jaribuni kusikiliza songi zake........achaneni na ile midude aliyokuwa akifakamia, kwani ktk verses zake hakuwahi kuitaja!! RIP shem

    ReplyDelete
  5. Nashukuru Michuzi kwa kuweka mambo sawa. Ila huyo repoter wa zamu inabidi awe makini na uletaji habari kuepuka kuwachanganya wasomaji. Hata hivyo tunashukuru kazi nzuri mnayoifanya kutujaza mambo mengi ya kitaifa na ya kimataifa!! Keep it up!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...