Waziri wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,Prof. Makame Mbarawa akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam (hawapo pichani) kuhusu usitishwaji wa matangazo ya Televisheni kwa kutumia Technolojia ya analogi na kuhamia teknolojia ya utangazaji ya dijitali ambao utasitishwa rasmi tarehe 31 Disemba mwaka 2012 saa sita kamili usiku. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk. Frorens Turuka.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Dk. Frorens Turuka akijibu maswali ya waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu usitishwaji wa matangazo ya Televisheni kwa kutumia Technolojia ya analogia na kuhamia teknolojia ya utangazaji ya dijitali ambao utasitishwa rasmi tarehe 31 Disemba mwaka 2012 saa sita kamili usiku. Kushoto ni waziri wa wizara hiyo Prof. Makame Mbarawa.Picha na Anna Itenda - Maelezo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Naomba Serikali, wanahari, wadau n.k iwasaidie wananchi ili kuepukana na ulaghai unaofanywa na wafanyabiashara kwa kuwauzia wananchi TV za Analog
    Nilisikia ya kwamba wau wa habari waliomba Serikali kuunganisha TV zote kwa kutoa king'amuzi kimoja ili kupunguza gharama na usumbufu. Je Waziri alilizungumzia hilo?

    ReplyDelete
  2. Huku Uk tulipewa miaka minne kujiandaa na hiyo ''swich over'' kutoka analogue kwenda digita. Hivi sasa ndiyo tunaanza kubadili kidogo kidogo kitongoji hadi kitongoji. Naona Tanzania kiboko kwa umahiri wa technologia, miezi tisa tu inatosha kufanya maandalizi husika na kubadili kila kitu. Hivi hiyo digita mtaipataje? kuna 'freeview' au mnalazimishwa ku-subscibe na kulipia?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...