Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri wa Masuala ya Jumuiya ya Madola, Umoja wa Mataifa na Afrika na Mazingira ( Parliamentary Under Secretary responsible for Africa, United Nations, economic issues, conflict resolution, and climate change) wa Uingereza,Bw Hendry Bellingham wakishuhudia Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernad Membe akiweka saini sambamba na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza kuhusu makubaliano kati ya nchi hizo mbili juu ya taratibu za kukabidhiana watuhumiwa wa uharamia na mali zilizokamatwa katika matukio ya uharamia katika bahari kuu leo February 23, 2012 Lancaster House, London. (PICHA NA IKULU)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. mwenzie anamuangalia yeye, membe anaangalia picha, haya bwana hicho tu kinawashinda ndiyo mtaweza kutuongoza kweli.

    ReplyDelete
  2. its funny that it is a one sided contract, because tanzania will never need uk to hand any pirates to them, but UK will need tanzania,

    if you know what I mean

    They should have gone to Tanzania to get that contract signed as it is for their benefit. It does not benefit us in anyway...

    ReplyDelete
  3. Hii ina maana hawa watuhumiwa watafungwa katika jela zetu???

    ReplyDelete
  4. kwahio picha ya Freddy Maro unaandika nani kapiga ila picha ya vekesheni unajifanya picha na Ikulu???

    ReplyDelete
  5. Kwanza niseme kuwa protokali za kupiga picha kama hii si kuangaliana, ila kuwaangalia waliopo kushuhudua utiaji sahihi kama vile wajumbe wa pande zote pamoja na waandishi wa habari. Kwa mantiki hii basi, Ndugu Membe mzee wa Mtama, was very right kuangalia upande wa picha, au wale waliokuwepo kushuhudia na bwa Hague alikosea kutowaangalia mashahidi kuonyesha kuwa, kweli tumekubaliana. Nakuombeni sana msiwe wepesi wa kurusha lawama kabla ya kuzifahamu protokali. Membe ni mwanadiplomasia aliyebobea sana. Miaka tisa akiwa Ubalozini Canada, miaka mitatu Washington, na pia akiwa anasomea masuala ya kidiplomasia pale John Hopkins alipokutana balozi wa kwanza wa korea hapa Tanzania bw jeong. Membe ni waziri wa mambo ya nje pekee aliyewahi kufanya kazi kwenye balozi zetu kama mshauri.
    Jifunzeni kuwa na heshima na viongozi wenu, hata kama mna tofauti. Mnapokuwa kuwa mbele ya mataifa mbali mbali, kiongozi wako hata kama hafai lazima kumpa heshima yeke.

    ReplyDelete
  6. hii nikuwakaribisha al shabaab kufanya vitu vyao tanzania sasa tujiandae ...kupokea kipigo na vile walivyokuwa wakiwafanyia kenya sasa vinakuja kwetu

    askari wa tanzania watakuwa nalakufanya pengine baada ya kusumbuwana sisi kwa sisi sasa kazi hiyoooooooo iko njiani mda sio mrefu .......kazi uliyoajiriwa sasa inakuja

    ReplyDelete
  7. wazungu mpaka leo wanatupa mikataba ya hajabu wafungwa wote wa kisomali wanataletwa katika jela za hapo bongo na itaifanya Tanzania kwa Accessible kwa ugaidi kutoka alshabab Bongo wameingizwa katika mkenge

    ReplyDelete
  8. Mdau Juu wa 2 umeongea kila pointi ya ukweli tunajizalilisha tu kwa uoga, Ukoloni haujafa unajionesha ndio unarudi kwa kasi. MZ

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...