Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 87 mpaka sasa

  1. tumewekwa mbali na marekani?

    yetu kubwa sana?

    ???

    ReplyDelete
  2. Ankal
    Bendera ya Tanzania imegeuzwa, mistari ya njano na nyeusi huwa inaanzia kwenye mlingoti na kushuka chini upande unaopeperushwa sana na upepo, kilichotokea ni kuwa kamba iliwekwa vibaya.

    ReplyDelete
  3. Bendera ya US iko kichwa chini miguu juu, bendera ya Bongoland iko migulubaja!

    ReplyDelete
  4. Bendera zote zimepauka isipokuwa ya Tanzania

    ReplyDelete
  5. Bendera yetu imewekwa chini juu. Na hili ni kosa ambalo limekuwa likirudiwa rudiwa sana hasa kwenye ofisi za kibalozi na taasisi za umoja wa mataifa. Wanaohusika watoe elimu hiyo!

    ReplyDelete
  6. flags are upside down!

    ReplyDelete
  7. Simple. Hizo nyingine tatu vibaraka wa hiyo ya kwanza.

    ReplyDelete
  8. USA flag, ipo nyumambele hahaha

    ReplyDelete
  9. Bendera ya marekani imegeuzwa upside down....by obamamtoto

    ReplyDelete
  10. mpandisha bendera ya tanzania alikuwa na haraka,imefuata upepo tuu. hahaaaa

    ReplyDelete
  11. Hivi hiyo bendera ya marekani haiko upside downkweli.

    ReplyDelete
  12. Hapo utagunduwa hiyo bendera ya Marekani imewekwa ndivyo sivyo (juu chini, kulia kushoto) na huo mlingoti mwingine ndo mtupu, hauna japo tambara.

    ReplyDelete
  13. bendera ya marekani iko juu chini,nyota hizo zinatakiwa kuwa juu

    ReplyDelete
  14. upside down

    ReplyDelete
  15. 1.)Bendera Hizo ni Za Marekani,Kenya,East Africa Community and Tanzania.....
    2.)Tatu kati ya Hizo zimepauka ya Tanzania tuu ndio Haijapauka
    3.)Bendera ya Marekani imegeuzwa iko juu chini
    4.)Milingoti ipo SITA.....

    ReplyDelete
  16. Bendela ya taifa la marekani imetundikwa juu chini

    ReplyDelete
  17. Nchi mbili za Jumuiya ya Afrika Mashariki bila kuwepo Uganda na badala yake kuna Bendera ya Marekani.

    ReplyDelete
  18. Duh! bendera yetu ya taifa ipo upside down! who is responsible????!!! ni aibu kweli!

    ReplyDelete
  19. Global 2012.February 14, 2012

    1.Mlingoti mmoja hauna bendera.
    2.Kuna bendera 4.Ya Marekani,ya kenya,ya hotel huska,na ya Tanzania kwa mfuatano.
    3.Bendera 2 ya Marekani na ya Tanzania zinapepea clock wise ie.kuelekea kulia na bedera 2 ya hotel husika na ya Kenya zinapepea ant clock wise ie.kuelekea kushoto
    4.Kuna milingoti ya bendera mitano.
    5.Bendera ya Kenya mlingoti wa tatu haija kusa kipivoti cha mlingoti.
    Asante.

    ReplyDelete
  20. kawatundika kichwa chini miguu juu wamarekani!

    ReplyDelete
  21. Bendera y a USA iko juu chini.

    ReplyDelete
  22. Nadhani bendera ya USA, Kenya na ya Tanzania zimegeuzwa juu chini!

    ReplyDelete
  23. hiyo bendera ya Marekani hicho kibox chenye nyota 52 hakikaagi hapo chini huwa kinakuwaga juu pembeni upande wa kushoto..... Mdau wa siku nying Texas USA

    ReplyDelete
  24. Hizi bendera zimetundikwa juu chini (zinaangalia chini)

    ReplyDelete
  25. Shija wa ShekilangoFebruary 14, 2012

    an "odd" combinations anyways, Minofu stars and stripes imepinduliwa kichwa chini mijuu guu! lol! Thanks

    ReplyDelete
  26. Bendera ya America imegeuzwa kichwa chini mijuu guu.

    ReplyDelete
  27. Bendera ya Marekani imegeuzwa. By ComWiz1

    ReplyDelete
  28. Bendera ya marekani iko upside down.heeee!

    ReplyDelete
  29. Bendara ya Tanzania imefungwa chini juu. Inaitwa kwa kimombo "Flag desecration" au Flag Abuse (bofya link hapo chini kwa habari zaidi)

    Kuna nchi ambazo zina sheria haswa inayosema bayana kuwa kuidhihaki bendera ya nchi hiyo ni kosa. Je Tanzania kitendo hicho ni cha kuvunja sheria? na ni sheria ipi haswa?

    Ankal, si ajabu kuwa mfunga bendera huyo wala hakujua kuwa amekosea kufunga bendera kwani elimu na ufahamu wetu wengi ni duni sana.

    http://en.wikipedia.org/wiki/Flag_desecration

    Alex bura, dar

    ReplyDelete
  30. Ze Benderaz upside down!

    ReplyDelete
  31. si useme tu kwani imekuwa chemsha bongo? Kuna mambo mengi kwenye picha:
    1. Milingoti miwili haina bendera;
    2. Bendera zilitakiwa ziwe za uganda, kenya, Tanzania, Rwanda na Burundi na marekani! za TZ, Ke, sijui, marekani na ipi vile?! ndiyo zipo;
    3. Tafsiri ya nbr 2 hapo juu malizia

    ReplyDelete
  32. nmegundua nguzo moja haina bendera

    ReplyDelete
  33. bendera imepinduliwa! Sioni ubaya li nchi lenyewe si la kupindua pindua tu kwani nani anajali?

    ReplyDelete
  34. bendera zote ziko upside down

    ReplyDelete
  35. upside down

    ReplyDelete
  36. Mambo mawili. Kwanza, bendera ya USA imewekwa miguu juu..maanake nchi imepinduliwa. Pili, nadhani jamaa alitumwa akaweke bendera ya U-ganda akaenda kuleta ya U-SA.

    Anonymous Allen Natai :)

    ReplyDelete
  37. Naweza kugundua kwamba mtoa mada ana "agenda" maana kuuliza tutagundua nini kunaashiria tayari muhusika amewaza kitu. Labda angetueleza amewaza nini alafu na siye tuchangie. Au siyo wadau?

    ReplyDelete
  38. Bendela ya marekani imegeuzwa juu chini

    ReplyDelete
  39. Bendera ya Tanzania imegeuzwa

    ReplyDelete
  40. Bendera ya nchi yangu Marekani imewekwa chini juu, na pia TZ japo ina bendera yake lakini si nchi ya kujivunia kutokana na uongozi mbaya.

    ReplyDelete
  41. Nimawazo yangu, nimegundua kwamba Tz niyamwisho kwa kila kitu

    ReplyDelete
  42. Bendera ya marekani imegeuzwa!

    ReplyDelete
  43. bendera ya marekani na kenya zinapepea lakini ya bongo imekataa kupepea nadhani imezingwa na bendera nyingine haipati upepo wa maana

    ReplyDelete
  44. bendera ya tanzania hiyo rangi ya buluu inatakiwa ikae juu na hiyo ya kijani ikae chini

    imegeuzwa.

    ReplyDelete
  45. Duuh jamaa wamegeuza bendera ya Marekani up side down. Ni vema wangeuliza kabla ya kupandisha bendera hizo endapo wangekuwa hawana hakika. Hayo ni makosa makubwa.

    ReplyDelete
  46. US Flag iko upside down

    ReplyDelete
  47. mkuu, bendera ya Obama haijawekwa sawa. It's upside down!

    ReplyDelete
  48. Nilijua wanakosea kwa kutotambua bendera ya nchi yao kumbe hata ya Marekani haitambuliki inakaa vipi kwa urahisi wake.

    Tupo tupo tu.

    ReplyDelete
  49. Huyu mtu aliyepandisha bendera hizi nadhani tayari alikuwa amepata chupa kadhaa za ulabu!au kama ana makengeza basi macho yake ni kama ya mijusi au ya kuku,haiwezekani bendera zote tatu za U.S.A, U.R.T na E.A.C ziwe upside down.Michuzi umetunyima haki ya kujua uzembe huu umetokea wapi,ilipaswa utujuze ili wahusika wawajibike au wawajibishwe kwa namna moja au nyingine

    ReplyDelete
  50. bendera ya Marekani iko kichwa chini au macho yangu tu sina uhakika

    ReplyDelete
  51. Bendera ya Marekani wameibanjua chini juu!

    ReplyDelete
  52. bendera ya marekani imewekwa juu chini, sehemu ya bluu na nyota nyeupe ilipaswa kuwa juu, ni kosa la kiitifaki

    ReplyDelete
  53. Bendera ya Marekani wameiweka kichwa chini miguu juu!. Kaaaazi kwelikweli.

    ReplyDelete
  54. BENDERA ZOTE ZIMEGEUZWA UPSIDE DOWN

    ReplyDelete
  55. Bendera inegeuzwa kichwa chini miguu juu ..............ndio maana inabidi turudishe JKT au mnasemaje wadau??

    ReplyDelete
  56. Naona bendera ya kenya imepauka na hiyo ya pili kutoka ya TZ choka mbaya,,na lingine upepo ulivuma kweli kweli na zikavuata mkondo..

    ReplyDelete
  57. Bendera ya Marekani imegeuzwa blue na hizo nyota zinatakiwa ziwe juu kushoto

    ReplyDelete
  58. flag ya U.S.A imegeuzwa up-side-down..

    ReplyDelete
  59. bendera ya bongo ina kasoro kwenye kamba

    ReplyDelete
  60. bendera ya bongo ina kasoro kwenye kamba

    ReplyDelete
  61. Bendera ya USA imewekwa juu chini. Nyota zinatakiwa ziwe juu na sio chini.

    ReplyDelete
  62. nimegundua kuwa aliyepandisha bendera anaundugu na OSAMA kwahiyo ameamua kuiweka kichwa chini bendera ya marekani.

    ReplyDelete
  63. nyota za bendera za marekani zinatakiwa ziwe juu na pia bobgo inaonyesha imeshika mkia pia kwenye milingoti

    ReplyDelete
  64. benderani zimegeuzwa chini juu?

    ReplyDelete
  65. Bendera ya America imegeuzwa.

    ReplyDelete
  66. Bendera ya Marekani imepinduliwa chini-juu.

    ReplyDelete
  67. american flag fly upside down!!! so funny!

    ReplyDelete
  68. american flag fly upside down!!! so funny!

    ReplyDelete
  69. Hahahaaaaaa!!!! Naona bendera ya Obama haija tendewa haki.....

    ReplyDelete
  70. naona huyo aliyopachika bendera ya marekani ana bifu nayo

    ReplyDelete
  71. duh!!!!! safi sana us flag juu chini chini juu

    ReplyDelete
  72. Mwenye hoja ya bendera, siku zijazo tafadhali badilisha Kiswahili ili iwe:

    UNAWEZA KUGUNDUA NINI KWENYE PICHA HII?

    Maelezo:
    Unapotumia kitenzi (verb) kilichofanyiwa unyambulishi (conjugation), na kisha kikawa kinafuatiwa na kitenzi kingine ambacho hakibadili kiambishi awali cha nafsi (subject prefix), basi inabidi kitenzi cha pili kibaki katika uhalisia wake (infinitive).

    Mfano:
    Ninapenda kusoma blogu.

    Siyo sahihi kusema:
    Ninapenda soma blogu.

    Lakini kwenye sentensi yangu ya kwanza pale juu ni sahihi kwa sababu:

    ... siku zijazo tafadhali badilisha ...

    Kitenzi "zijazo" kinabeba kiambishi awali cha nafsi ya nomino "siku" ambacho ni "zi" wakati kitenzi cha pili "badilisha" hakina muundo unaoanza na "ku" wala kiambishi nafsi kwa kuwa chenyewe kiko katika mfumo wa "amri" (imperative)inayopoozwa na neno tafadhali.

    Aidha, haiwezekani kusema"kubadilisha" kwa kuwa hiki kitenzi kinamhusu mhusika anayepewa ujumbe, na siyo nomino "siku".

    Kitenzi cha pili kingeweza kuwa "ubadilishe" iwapo ningetaka kutumia amri ya upole moja kwa moja (kama ilivyo kwenye subjunctive), lakini si lazima.

    Nimeahidi mahali fulani kwamba nitakuwa natoa masomo ya namna hii kila linapotokea kosa na nikaliona ili kuiepusha nchi yetu na tatizo kama tulilonalo kwenye Kiingereza. Tutakuwa taifa la ajabu mno. Sidhani kama tuna sababu ya kuwa na Kiswahili kibovu kama Wakenya.

    Msomaji atakayehitaji msaada zaidi, aniandikie:
    Mobhare Matinyi,
    matinyi@hotmail.com.

    ReplyDelete
  73. bendera ya Marekani iko juu chini (up side down). I hope this is not in TZ!...
    Ndugu AF.

    ReplyDelete
  74. Bendera ya US imegeuzwa, chini juu.

    ReplyDelete
  75. nimegundua kuwa, mlingoti wa kwanza hauna bendera ni hayo tu!

    ReplyDelete
  76. Mi nimegundua kuwa kulikuwa na upepo mkali sana.

    Mdau Norway.

    ReplyDelete
  77. BENDERA YA IVORYCOAST IKO NUSU MLINGOTI TEH TEH TEH.

    ReplyDelete
  78. MNH JAMANI TUKUMBUKE HILO LA KUGEUZA UPSIDE DOWN BENDERA ZA WATU LILIMGHARIMU MZEE OBAMA MWAKA JANA KWA KUWAALIKA MARAISI KTK MKUTANO FULANI HUKO USA NA KWA BAHATI MBAYA AU KUTOKUJUA BENDERA YA UFILIPINO IKAWEKWA UPSIDE DOWN,YULE SIJUI ALIKUWA RAISI AU MUWAKILISHI WAKE ALIMUAMBIA OBAMA KUFANYA HIVYO TAFSIRI YAKE KWA HUKO KWAO NI KWAMBA NCHI IPO VITANI,ILIBIDI OBAMA AOMBE RADHI HADHARANI KWA KOSA HILO,SASA HAPA KWETU SIJUI WENYE BENDERA WATASEMAJE KUHUSU HILO ILA WAMAREKANI NAFIKIRI HAWAMAINDI SANA ILA KWA ANGALIZO TU TUWE MAKINI KWANI KUNA MATAIFA MENGINE NI WAKOROFI HATA KWA KOSA DOGO INGAWA LINAWEZA KUWA KUBWA JK ANAWEZA KUAMBIWA AOMBE RADHI

    ReplyDelete
  79. wewe MOBHARE MATINYI kachunge ng'ombe achana na kiswahili cha kwenye blogu,au kama unajua kiswahili nenda mashuleni na vyuoni kafundishe hapa si mahali pa kufundishana lugha unless mtu aombe msaada huo

    ReplyDelete
  80. kuna milingoti sita.miwili haina bendera.
    bendera ya marekani ip upside down.kuna upepo unaoelekea upande tofauti na uelekeo wa bendera.hivyo bendera zinapepea uelekeo tofauti na uliotarajiwa.

    ReplyDelete
  81. USA and Bongo Flags are upside down

    ReplyDelete
  82. Picha imewekwa kinyume ingekuwa enzi zile za picha za mikanda (film cameras) tungesema umegeuza 'negative' wakati wa kusafisha!

    ReplyDelete
  83. mkandamizajiFebruary 15, 2012

    1. Upepo mkali umezielekeza bendera upande mwingine.

    2. Bendera za Tz na USA zimekosewa.

    3. Aliyepandisha bendera ni mfanyakazi wa EAC therefore ni mkenya, ndo maana kapatia ya kenya na ya EAC na kaziweka juu-chini za TZ na USA.

    4. Wabongo wengi hatuna la kufanya ndo maana tunapoteza muda kuchambua yasiyo na msingi, na yale yenye msingi hatujacomment kabisa (tazama idadi ya comments kwenye articles zingine za blog hii)

    5. Sijui nafanya nini hapa...

    ReplyDelete
  84. Mlingoti wa kwanza una bendera ya Ivory cost lakini haikonekani ktk hii picha kwa sababu inapepea nusu mlingoti tokana na kipigo toka kwa zambia afcon 2012.

    ReplyDelete
  85. Nyie mnaosema bendera ya tz iko juu chini mmeiona wapi? mbona mnapenda kuikandia inchi yetu? Ya usa ndio imegeuzwa.

    ReplyDelete
  86. Michuzi
    Najua una tabia za kunitia kapuni, na pia naona nimechelewa kidogo kuweka maoni yangu kwenye habari hizi za bendera ya mericani.Kuna jamaa wamesema kuwa ni funny.Wajulishe wadau inawezekana kuwa bendera hapo juu ilikuwa upside down by mistake. Lakini bendera yako kuwa upside down ni namna ya SOS, yaani kuomba msaada kwenye matatizo makubwa."It signify dire distress...extreme danger to life" Flag code.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...