Mhe. Job Ndugai, Mb na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akijiandaa kuongoza kikao cha pamoja cha wabunge toka nchi za Afrika, Caribbean na Pacific kinachofanyika jijini Brussels kuanzia jana. Katika kikao hicho Mhe. Naibu Spika alianza rasmi nafasi yake ya uenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Jamii na Mazingira ambayo ataishikilia kwa miaka miwili ijayo. Mhe. Naibu Spika ataongoza kamati hiyo iliyoko kwenye jumuiya ya nchi za Afrika, Caribbean na Pacific ambayo ina jumla ya nchi wanachama 79. Wa pili kulia ni Mbunge toka Tanzania, Mhe. Dr. Mary Mwanjelwa ambae pia anashiriki mkutano huo.
Mhe. Naibu Spika akiwa na balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji aliemaliza muda wake, Mhe. Balozi Mlay (katikati) katika picha ya pamoja na Afisa wa Ubalozi huo Bw. Cheche mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Kamati ya Masuala ya Jamii na Mazingira.Picha na Saidi Yakubu,Brussels.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...