Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ameagana na mabalozi wapya watatu watakaoiwakilisha Tanzania nchi za nje.Mabalozi waliokwenda ikulu kumuaga Rais Kikwete ni pamoja na Dkt.James Msekela anayekwenda Italia, Dkt.Ladislaus Komba anayekwenda Uganda na Mhe.Bi.Shamim Nyanduga anayekwenda Msumbiji. Pichani  Rais   Kikwete akizungumza na Balozi Mpya wa Tanzania nchini Italia Dkt.James Msekela ikulu jijini Dar es Salaam leo
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Uganda,Dkt.Ladislaus Komba ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na balozi Mpya wa Tanzania nchini Msumbiji Mhe. Shamim Nyanduga ikulu jijini Dar es Salaam leo. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. yaani siku hizi mtu akichaguliwa balozi then anaanza ziara ya miezi sita kuaga?? Guys, Serikali haina hela jamani hebu acheni kuleta mzaha!!
    Che

    ReplyDelete
  2. Huyu Che katoka wapi? Anaonyesha ujinga wake wa diplomasia. Diplomasia lazima izingatie hali ya nyumbani anapotoka mwanadiplomasia, hivyo lazoma kumfunda kabla hajaenda huko anapotumwa ili akiongelea kilimo anajua hali yetu na mahitaji yake, akiongelea ajira anajua hali ya vijana wetu, vile vile utalii. Kila kitu sharti uwekeze kwanza ili wanadiplomasia wako wawe mahiri na makini!!

    ReplyDelete
  3. balozi hutumikia kipindi cha miaka 4.baada ya hapo anaweza kuongezewa. sasa hawa miezi 6 tayari wametumia hapa nyumbani. je, utumishi wao utahesabika tangu wameteuliwa au tangu wafike ktk vituo vya kazi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...