

(PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Wazee wangu, nafahamu jinsi gani mlivyo na moyo wa huruma kwa vijana waliofungiwa. Hii inaonyesha ni jinsi gani mnavyojali mpira wa miguu. Lakini mpira una sheria zake. Kila kosa linalofanywa na waamuzi, wachezaji, waalimu na hata wamiliki wa timu, lina adhabu zake. Katika adhabu zote zinazohusiana na mpira wa miguu, hakuna ngumi. Tayari hawa vijana wenu wameshasamehewa. Vinginevyo ilikuwa wafunguliwe mashtaka na kama wakipatikana na hatia, basi wangetumikia kifngo kisichopungua miaka miwili. Nafikiri ni vizuri waendelee kutumikia adhabu waliyopata ili iwe fundisho kwao na kwa wachezaji wengine. Wachezaji wanaruhusiwa kumzonga mwamuzi lakini siyo kumpiga. Kama tunapenda mpira wa miguu, basi ni lazima tunzingatie sheria zake. Pia kama tunapenda kuvunja sheria lakini hatupendi adhabe zake, basi tukubali kuwa mpira umetushinda. Hata kama mwamuzi alifanya kosa la kutisha, hakutakiwa kupigwa ngumi. Ni hayo tu wazee wangu.
ReplyDeleteHawa wazee mbona hawajalaani kitendo cha kihuni walichofanya wachezaji? Busara zao zingewatuma kwanza kulaani kuliko kuibuka tu na kuwaombea msamaa. Kutolaani maana yake ni kuwaunga mkono wachezaji sasa sijui mtu anayeunga mkono uhuni kama anastahili kusikilizwa.
ReplyDeleteMasikini Mzee heri alikolala. Yanga imeingiliwa.
ReplyDeletekwanza mm naona wangeongezewa adhabu hasa yule kijana aliyefungiwa mwaka 1 pamoja na cannavaro..wapuuzi sana hawa..mim kwa kusema ukweli ni mpenzi wa simba wa msimamo wa kati tu lakin napenda haki zaidi kuliko hio simba..nilipenda sana mpira zamani kuliko sasa...lakini huyo kijana aliyempiga refa,nasema si kwa vile simpenda kwa sababu ni wa timu pinzani,hapana ni kwa sababu hana adabu kwa asilimia 100 nadhani..TFF wakae upya na kumwongezea adhabu pamoja na faini kabisa.
ReplyDeleteupande mwingine, TFF pia wasiishie kusema wanampongeza tu kapteni wa timu ya yanga kwa kuwasihi wenzake waache fujo..inapaswa apewe na yeye pongezi ya chochote na si maneno matupu kwa maneno matupu hayavunji mfupa jamani..apewe hongera ya kiasi chochote cha fedha kwa mfano ili iwe motisha kwa yeye binafsi na wengine siku za usoni...kama hilo haliwezekani basi na hawa wengine wasipewe adhabu ya faini ila wafungiwe tu
huo ni mtazamo wangu tu
hsm
Hivi baraza la wazee wa Yanga ni chombo halali na kina uwakilishi wake moja kwa moja TFF? Huu ni ukurupukaji, Nadhani hili baraza linatambulika ndani ya klabu yao tu na halina nguvu ya kisheria ya kuagiza TFF. Kikubwa wanachoweza kukifanya ni kuushauri uongozi wa timu yao na wao ndio wanaoweza kuongea na TFF? Hivi ukiwa mzee ndo wa kutumika kuhalalisha makosa na kupindisha sheria? Tatizo la Tanzania saivi kila kitu wanaiga kutoka kwenye siasa. Shame on you Yanga
ReplyDeletemtoa maoni huyo wa kwanza na penda kukupongeza kwa lugha ya heshima uliyoa waelezea wazee wetu pia na maelezo yako . Kiukweli vitendo walivyo fanya hao wanaojiita wachezaji kinasikitisha , hasa kwa jamii ikiwa wao kama kioo adhabu waliopewa inawafaa kwani itawaumiza kiuchumi na itawafanya wakumbuke nidhamu
ReplyDeleteNakubaliana na mdau aliyesema kuwa wazee hawa walipaswa kwanza kulaani uhuni uliopindukia uliofanywa na wachezaji wa Yanga kabla ya kuomba wapunguziwe adhabu pamoja na kwamba adhabu waliopewa bado ni ndogo kulingana na makosa waliofanya.
ReplyDeletekejeli kejeli 2, yeboyebo mnalo mwaka huu!
ReplyDeleteMnakua kama Boom FC au Ashanti khaa!
Mi naona timu nzima na mashabiki wao wangepewa adhabu ya kutotumia Uwanja wa Taifa kwa msimu mzima maana wametuharibia hata sehemu za kukaa timu gani ina mashabiki kama wanachama wa Al-Shababu? au kwasababu hizo nguo zenu zina rangi ya chama tawala basi mnaona na nci hii mmeitawala nyanja zote?adhabu haitoshi TFF waongezeeni zaid na zaid!
ReplyDeleteNyie wazee shukuruni kuwa hao wahuni mnaowatetea wamepewa adhabu ndogo. Mwasika pamoja na kufungiwa mwaka mmoja alitakiwa kufunguliwa shitaka la kushambulia (assault) ambalo lingempeleka jela si chini ya miaka miwili. Kwa wale wanaokumbuka, Eric Cantona alihukumiwa kifungo jela baada ya kumtwanga shabiki wa timu pinzani mwaka 1995. Adhabu hiyo ilifutwa baada ya Cantona kukata rufaa. Hii ni mbali ya adhabu ya kufungiwa miezi minane na FA. Baadaye Fifa iliifanya adhabu hiyo kuwa ni ya dunia nzima ikimaanisha kuwa Cantona hakuweza kuikwepa kwa kuhamia klabu ya nchi nyingine. Manchester United tayari ilishamfungia Cantona miezi minne na kumpiga faini ya pauni 20,000. Huku ndiko kusimamia sheria za mchezo na kudumisha nidhamu, lakini Bongo tunatetea ujambazi katika soka halafu tunategemea tufanye vizuri katika michuano ya kimataifa.
ReplyDelete