Basi la daladala linalofanya safari kati ya Ubungo na Tegeta, Dar es Salaam, likisimamishwa ili liungane kwenye mgomo ulioitishwa na madereva na makondakta wa daladala hizo leo kupinga kitendo cha kulipishwa tozo nyingi katika kituo cha daladala cha Ubungo Tanesco.
Daladala zinazofanya safari kati ya Ubungo-Tegeta, Dar es Salaam, zikiwa zimeegeshwa katika kituo cha njia panda ya kwenda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam jana, baada ya madereva na makondakta kugoma wakidai kulipishwa tozo nyingi katika Kituo cha Daladala cha Ubungo na kutojua fedha hizo zinakopelekwa. Kwa siku hulipa kwanza sh. 1,500 na  500 halafu kila linapofika kupakia abiria hulipishwa sh 400. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
 Mmoja wa madereva wa zaidi ya daladala 100 zilizogoma, akijielezea unyanyasaji huo 
 Daladala ikisimamishwa kuungana na wenzao waliogoma
Abiria wakiwa wamekata tamaa ya kupata usafiri wakati Daladala zinazofanya safari kati ya Ubungo-Tegeta, Dar es Salaam,  madereva na makondakta wake kugoma wakidai kulipishwa tozo nyingi katika Kituo cha Daladala cha Ubungo na kutojua fedha hizo zinakopelekwa. Kwa siku hulipa kwanza sh. 1,500 na  500 halafu kila linapofika kupakia abiria hulipishwa sh. 400. (PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Abiria wanateseka lakini kama itasaidia kuondoa ufisadi/rushwa wamefanya jambo la maana.

    ReplyDelete
  2. Rais alishasema wakigoma wenye daladala tutembee, shida iwapi? Wagome mpaka mwisho...au nao wanataka mtu ajiuzulu?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...