Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Nyayo Za Mama inayojishugulisha na sanaa ya uchoraji na kunakshi picha ya Nyayo Za Mama, Candida Bahame (kushoto)akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Ujamaa Art Gallery Lona Mashiba wakati wa ufunguzi wa maonesho ya mauzo ya kazi z sanaa za Mama Bahame yanayoendelea katika Gallery hiyo iliyopo Mbuyuni njia ya Mwenge
Mkurugenzi Mtendaji wa Ujamaa Art Gallery Lona Mashiba (wa kwanza) akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Wakimbizi (UNHCR) Chansa Kapaya wakiangaliwa picha zilizochorwa na mchoraji Candida Bahame.

Na Mwandishi Wetu

WANAJAMII wametakiwa kutumia kazi za sanaa za mikono za wasanii wa hapa nchini katika kupamba nyumba zao ili kuongeza hamasa na maendeleo ya tasnia hiyo hapa nchini.

Wito huo ulitolewa na Mdau wa sanaa za uchoraji Candida Bahame ambae ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Nyayo Za Mama wakati akizindua maoenesho ya wiki mbili ya kazi zake za sanaa.

Candida alisema kuwa wasanii wa hapa nchini wanao uwezo wa kuchora na kutengeneza picha kwa kutumia viashiria mbalimbali vya kisanii ambavyo zinapendezesha nyumba.

Alisema kuwa wanajamii wakiwa na utamaduni wa kununua kazi zao za sanaa na kuzipamba majumbani kwao watakuwa kwa kiasi kikubwa wamesaidia kukua kwa sanaakiwa kama mdau wa kazi za sanaa ya uchoraji hapa nchini.

“ Mimi naona kuwa muda umefika kwa hoteli zetu, ofisi na hata nyumba zetu watu kutumia picha za wasanii wa hapa nchini katika kupamba nyumba zao ili kuonesha kuwa wanathamini na kutambua sanaa zetu hapa nchini” alisema Candida.

Akizungumzia sanaa yake hiyo ambayo alisema kuwa alianza tangia miaka ya 1980, Candida alisema kuwa gharama ya picha zake anazipanga kulingana na muda aliotumia kuzichora pamoja na umaridadi wa picha hizo.

Alisema kuwa anatumia kipaji chake kufikisha ujumbe kwa njia ya maneno ambapo anatumia shanga kushona maneno yenye ujumbe na pia anatumia shanga kutengenezea picha.Maonesho hayo ya wiki mbili yanaendelea katika Ujamaa Art Gallery.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Naomab website ya huyu dada.

    ReplyDelete
  2. Hongera sana Candida, very impressive work, I'll surely make a point of visiting your gallary.

    Amina.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...