Steve Annu, mpiga picha mpya wa Globu ya Jamii, amekamata taswira kadhaa jioni hii kuionesha jinsi mvua kubwa iliyonyesha toka milango ya saa tisa hivi iliyoleta mafuriko sehemu mbalimbali ambazo mitaro yake ina kwikwi. 

Taswira hizi ni za Mikocheni kati ya Tanesco na Shoppers Plaza ambako pamekuwa kero kutokana na mitaro yake kutofanyiwa kazi miaka nenda miaka rudi. Wakati huo huo tishio la Tsunami ambalo lilileta wasiwasi kwa wakazi wengi wa jiji la Dar na kwingineko limeinuliwa baada ya tetemeko kubwa huko Indonesia. 

Tamko rasmi la Idara ya Hali ya Hewa Tanzania limetolewa Bungeni Dodoma muda mfupi uliopita kuthibitisha kwamba hali imeanza kutengamaa baada ya tishio hilo kupita, na kutoa rai kwamba vyombo vya usafiri majini hususan katika Bahari ya Hindi wasubiri  hadi kesho asubuhi  kabla ya kuendelea na shughuli zao, na kwamba hakuna habari za madhara ya watu ama mali zao hapa nchini. Globu ya Jamii inafuatilia kwa karibu swala hili
 Maji kila mahali
 Tutafika tu kwa Kudra zake Mola
 Hii sasa balaa
 Moka zikivaliwa baada ya kuvuliwa kutokana na mvua
 Kufa kufaana
 Balaa
 Mafuriko
 Twende mbele...
 Bora kufika salama
 Leo kazi ipo
Hii adha hapa Mikocheni itaisha lini toba....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. mwe!mwe! hii ni bongo tambarare ya kina ras makunja,kesho ajuae mungu,
    Bongo tambarare

    ReplyDelete
  2. Dah! poleni sana Dar es salaam. Hali inatisha mno.

    ReplyDelete
  3. hili eneo mikocheni ilibidi liwe wazi hadi milele

    eneo la kupata chumvi eneo la mabwawa ya chumvi eneo ytangu miaka ya 80's wakati hakuna majumba hayo palikuwa panajaa maji sema kulikuwa na mifereji maji yanaenda baharini

    sasa serikali imeruhusu watu kujenga mifereji imezibwa mtategemea nini hapo?

    kuvunja waliopewa vibali kwa rushwa ndio solution

    ReplyDelete
  4. Nafikiri wakati umefika kuweka sheria inayokataza mtu mzima kubebwa kuvushwa barabarani kwasababu ya kukwepa maji. Zanzibar baada ya mapinduzi tulipiga marufuku kutumiwa kwa Ma-"rickshaw" kwasababu yanamzalilisha mtu.

    ReplyDelete
  5. Poor sewage planning

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...